-
Je, Unatoa Mrudisho wa Utukufu wa Yehova?Mnara wa Mlinzi—2012 | Mei 15
-
-
7. Ni lazima tutambue nini kuhusu hali yetu ili tutoe mrudisho wa utukufu wa Mungu?
7 Ili kuwa katika hali nzuri ya kutoa mrudisho wa utukufu wa Mungu, ni lazima tutambue kwa unyoofu hali yetu ya dhambi. (2 Nya. 6:36) Tunahitaji kutambua mielekeo yetu ya dhambi na kujitahidi kuidhibiti ili tuweze kufanya maendeleo ili hatimaye tuweze kumtukuza Mungu kikweli. Kwa mfano, ikiwa tumetumbukia katika dhambi yenye kuaibisha ya kutazama ponografia, ni lazima tukubali ukweli wa kwamba tunahitaji msaada wa kiroho, na kwamba tunapaswa kuchukua hatua ya kuupata msaada huo. (Yak. 5:14, 15) Hiyo ni hatua ya kwanza tunayopaswa kuchukua ikiwa tunataka kuwa na maisha yanayomheshimu Mungu kikamili. Tukiwa waabudu wa Yehova, ni lazima tuendelee kujichunguza wenyewe ili kujua ikiwa tunatimiza viwango vyake vya uadilifu. (Met. 28:18; 1 Kor. 10:12) Hata tuwe na mielekeo gani ya dhambi, ni lazima tuendelee kupambana nayo ili tuweze kutoa mrudisho wa utukufu wa Mungu.
-
-
Je, Unatoa Mrudisho wa Utukufu wa Yehova?Mnara wa Mlinzi—2012 | Mei 15
-
-
17. Tunafaidika jinsi gani tunapotambua kwamba hatuwezi kutoa mrudisho wa utukufu wa Mungu kwa ukamili?
17 Ulimwengu kwa ujumla hautambui uzito wa dhambi, lakini sisi tunatambua. Jambo hilo linatufanya tutambue uhitaji wa kupambana na mielekeo yetu ya dhambi. Kutambua hali yetu ya dhambi kunatuwezesha kuizoeza dhamiri yetu hivi kwamba itatuchochea kutenda kwa njia inayofaa wakati tamaa ya kutenda dhambi inapoanza kusitawi akilini na moyoni mwetu. (Rom. 7:22, 23) Ni kweli kwamba huenda tukawa dhaifu, lakini Mungu anaweza kutuimarisha ili tufanye yaliyo sawa katika hali yoyote ile.—2 Kor. 12:10.
-