-
Yule Ambaye Manabii Wote WalimshuhudiaMwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
-
-
11. Eleza jinsi ambavyo dhabihu ya Yesu inaweza kutufaidi sana.
11 Fidia hiyo inatufaidi kwa njia nyingine hata sasa. Kwa mfano, tujapokuwa watenda-dhambi, dhabihu ya Yesu inatuwezesha kuwa na dhamiri safi kwa sababu ya kusamehewa dhambi zetu. Dhabihu za wanyama ambazo Waisraeli walitoa kulingana na Sheria ya Musa hazingeweza kufanya hivyo. (Matendo 13:38, 39; Waebrania 9:13, 14; 10:22) Lakini ili tusamehewe, ni lazima tutambue kwa unyofu kwamba tunahitaji sana dhabihu ya Kristo: “Ikiwa twatoa taarifa: ‘Sisi hatuna dhambi yoyote,’ tunajiongoza wenyewe vibaya na kweli haimo katika sisi. Ikiwa twaungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na mwadilifu hata kutusamehe dhambi zetu na kutusafisha ukosefu wote wa uadilifu.”—1 Yohana 1:8, 9.
-
-
Yule Ambaye Manabii Wote WalimshuhudiaMwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
-
-
13. Tunapaswa kufanya nini tukitambua kwamba tumetenda dhambi, na kwa nini?
13 Bila shaka, bado tutakuwa na tabia fulani zenye dhambi hata baada ya kubatizwa. Tufanye nini? Mtume Yohana alisema: “Nawaandikia nyinyi mambo haya ili msifanye dhambi. Na bado, ikiwa yeyote afanya hasa dhambi, tuna msaidiaji kwa Baba, Yesu Kristo, aliye mwadilifu. Na yeye ni dhabihu yenye kufunika kwa ajili ya dhambi zetu.” (1 Yohana 2:1, 2) Je, hilo linamaanisha kwamba hata tukifanya dhambi gani, Mungu atatusamehe tukimwomba msamaha? Si lazima. Msamaha unategemea toba ya kweli. Huenda pia tukahitaji msaada wa Wakristo wakomavu wenye uzoefu kutanikoni. Ni lazima tukubali kosa letu na kujuta kikweli ili tuweze kujitahidi kabisa kutolirudia tena. (Matendo 3:19; Yakobo 5:13-16) Tukifanya hivyo, tunaweza kuwa na hakika kwamba Yesu atatusaidia na tutapata tena kibali cha Yehova.
-