-
Mwimbieni Yehova!Mnara wa Mlinzi—2010 | Desemba 15
-
-
Unaweza Kuonyesha Uthamini Wako
17. Ni mawazo gani yanayoweza kutusaidia tusiogope kuaibika wakati kutaniko linapoimba?
17 Je, tunapaswa kuogopa kuimba kwa sauti katika mikutano ya Kikristo kwa sababu tunaogopa kuaibika? Fikiria jambo hilo kwa njia hii: Je, si ni kweli kwamba “sisi sote hujikwaa mara nyingi” tunapozungumza? (Yak. 3:2) Hata hivyo, hatuogopi kumsifu Yehova nyumba kwa nyumba eti kwa sababu maneno yetu si makamilifu. Basi kwa nini, tuogope kumsifu Mungu kwa nyimbo kwa sababu sauti zetu si kamilifu? Yehova, “aliyekifanya kinywa kwa ajili ya mwanadamu,” anafurahi kusikiliza tunapotumia sauti zetu kuimba sifa zake.—Kut. 4:11.
18. Toa mapendekezo yanayoweza kutusaidia kujifunza maneno ya nyimbo zetu.
18 CD zenye kichwa Mwimbieni Yehova—Muziki wa Kuimbwa zimetayarishwa katika lugha mbalimbali. CD hizo zina nyimbo mpya ambazo zimeimbwa kwa vyombo vya muziki na pia kikundi cha waimbaji. Kusikiliza muziki huo kunafurahisha sana. Sikiliza muziki huo mara nyingi; ukifanya hivyo utajifunza haraka maneno ya nyimbo chache mpya. Nyingi kati ya nyimbo hizo zina maneno ambayo yametungwa kwa njia ya kwamba unapoimba mstari mmoja, inakuwa rahisi zaidi kuimba mstari unaofuata. Basi unaposikiliza CD hizo, kwa nini usijaribu kuimba ukifuatana na waimbaji? Ukielewa vizuri maneno na muziki huo nyumbani, bila shaka utaweza kuimba kwa uhakika zaidi kwenye Jumba la Ufalme.
-
-
Mwimbieni Yehova!Mnara wa Mlinzi—2010 | Desemba 15
-
-
20. Umeazimia kufanya nini?
20 Yehova anakazia uangalifu nyimbo zetu za sifa. Ni za maana kwake. Tunaweza kuufanya moyo wake ushangilie kwa kuimba kwa sauti na kwa moyo wetu wote kila mara tunapokutana ili kuabudu. Ndiyo, iwe sisi ni waimbaji stadi au wenye kujifunza, acheni ‘tumwimbie Yehova’!—Zab. 104:33.
-