Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi ya Kupata Shangwe Kutokana na Zawadi ya Useja
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
    • Loli ambaye ametumikia akiwa painia kwa miaka 14 anasema hivi: “Upainia unanisaidia kuwa na kusudi maishani. Nikiwa dada mseja, ninatumika kwa bidii na nina shughuli nyingi maishani. Na hilo linanisaidia kuepuka upweke. Mwishoni mwa siku ninahisi nimetosheka kwa sababu ninaweza kuona kwamba huduma yangu inawasaidia sana watu. Hilo linaniletea shangwe nyingi sana.”

      Dada wengi wamejifunza lugha mpya, na wamepanua huduma yao kwa kuwahubiria watu wanaozungumza lugha za kigeni. Ana, aliyetajwa mwanzoni anasema hivi: “Katika mji ambamo ninaishi, kuna maelfu ya wageni.” Anafurahia kuwahubiria watu wanaozungumza Kifaransa. “Kujifunza lugha ambayo ninaweza kuitumia kuzungumza na wengi wao kumenifungulia njia ya kutumika katika eneo jipya na hilo limefanya kazi yangu ya kuhubiri ipendeze sana.”

      Kwa kuwa mara nyingi waseja hawana madaraka mengi, wengine wao wamejitolea kutumika katika maeneo yenye uhitaji mkubwa zaidi wa wahubiri. Lidiana, dada mseja mwenye umri wa miaka 30 na kitu, ambaye ametumikia katika nchi zenye uhitaji mkubwa zaidi anasema: “Ninaamini kabisa kwamba kadiri unavyofanya mengi zaidi katika utumishi wa Yehova, ndivyo inavyokuwa rahisi zaidi kupata marafiki wa karibu na kuhisi unapendwa. Nimepata marafiki wengi wa karibu kutoka katika nchi na malezi mbalimbali, na marafiki hao wamefanikisha sana maisha yangu.”

  • Jinsi ya Kupata Shangwe Kutokana na Zawadi ya Useja
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
    • Loli anasema hivi: “Popote ninapoenda, ninatafuta marafiki wa kweli kutanikoni ambao watanipenda na kunitegemeza ninaposhuka moyo. Ili kuimarisha urafiki huo, ninajitahidi kupendezwa na wengine na kuwaonyesha upendo. Nimetumikia katika makutaniko manane, na sikuzote nimepata marafiki wa kweli. Mara nyingi si dada wa umri wangu, nyakati nyingine ni mama waliozeeka au matineja.”

  • Jinsi ya Kupata Shangwe Kutokana na Zawadi ya Useja
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
    • Lidiana anasema: “Ninaishi maisha yenye kuridhisha ambayo yanategemea utumishi wangu na uhusiano wangu pamoja na Yehova. Ninajua watu waliofunga ndoa ambao wana furaha na wengine ambao hawana furaha. Jambo hilo hakika linanisadikisha kwamba furaha yangu haitegemei kuolewa au kutoolewa wakati ujao.”

  • Jinsi ya Kupata Shangwe Kutokana na Zawadi ya Useja
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
    • Carmen, dada mseja mwenye umri wa miaka 40 hivi anasema: “Ninafurahia hali yangu jinsi ilivyo, sioti ndoto kuhusu mambo nisiyokuwa nayo.”

  • Jinsi ya Kupata Shangwe Kutokana na Zawadi ya Useja
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
    • Ester, dada mseja mwenye umri wa miaka 30 na kitu anasema hivi: “Ninafikiri siri ya kupata furaha ni kukazia fikira mambo mazuri katika hali yoyote unayokabili.” Carmen anaongezea hivi: “Ninaamini kwamba hata nikiolewa au nisipoolewa, nikitanguliza mambo ya Ufalme, Yehova hataninyima jambo lolote jema.” (Zab. 84:11) “Huenda maisha yangu hayako kama vile nilivyopanga, lakini nina furaha na nitaendelea kuwa na furaha.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki