Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mashauri ya Hekima Kuhusu Useja na Ndoa
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Oktoba 15
    • 7. Toa mfano wa Mashahidi waseja ambao wametumia hali yao ya useja kuendeleza kazi ya Ufalme.

      7 Wakristo wengi waseja wanatumia hali yao ya useja kutimiza mengi katika kazi ya Ufalme. Sara na Limbania, ambao ni mapainia waseja huko Bolivia, walihamia katika kijiji ambacho hakikuwa kimehubiriwa kwa miaka mingi. Je, ukosefu wa umeme ungekuwa tatizo kwao? Walisema hivi: “Hakuna redio au televisheni, hivyo watu hawakengeushwi wasifanye jambo wanalopenda kufanya wanapostarehe, yaani, kusoma.” Wanakijiji fulani waliwaonyesha mapainia hao vitabu mbalimbali vya Mashahidi wa Yehova ambavyo walikuwa bado wanasoma lakini vitabu hivyo havichapishwi tena. Dada hao walipata watu wanaopendezwa katika karibu kila nyumba, hivi kwamba hawakuweza kuwatembelea watu wote katika eneo hilo. Mwanamke mmoja mzee aliwaambia hivi: “Lazima mwisho uwe umekaribia kwa sababu Mashahidi wa Yehova wametufikia hatimaye.” Baada ya muda mfupi, watu fulani katika kijiji hicho walianza kuhudhuria mikutano ya kutaniko.

  • Mashauri ya Hekima Kuhusu Useja na Ndoa
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Oktoba 15
    • 9 Dada mmoja mseja kutoka Marekani ambaye ni painia aliandika hivi: “Watu fulani wanaamini kwamba waseja hawawezi kupata furaha. Lakini nimeona kwamba furaha ya kudumu inategemea uhusiano wa mtu pamoja na Yehova. Ingawa maisha ya useja ni ya kujidhabihu, ni zawadi nzuri ajabu ukiitumia vizuri.” Aliandika hivi kuhusu kupata furaha: “Badala ya kumzuia mtu kupata furaha, useja unaweza kumsaidia kupata furaha. Ninajua kwamba Yehova anawapenda kwa wororo watu wote, waseja na waliofunga ndoa.” Sasa dada huyo anatumikia kwa furaha katika nchi ambayo ina uhitaji mkubwa zaidi wa wahubiri wa Ufalme.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki