-
Kwa Msaada wa Yehova, Tuliokoka Serikali za KimabavuMnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 1
-
-
Baada ya miezi michache, Wanazi walilazimika kukimbia haraka kutoka kambini kwa sababu ya wanajeshi wa Urusi waliokuwa wakikaribia. Tulipokuwa tukijitayarisha kuondoka, sisi akina ndugu—huku tukihatarisha uhai wetu—tuliamua kwenda kwenye kambi za wanawake ili kuona hali ya dada zetu 20 hivi wa kiroho waliokuwamo, kutia ndani Elsa Abt na Gertrud Ott.b Walipotuona, walitukimbilia haraka na baada ya kutiana moyo kidogo pamoja nao, waliimba wimbo wa Ufalme ambao ulikuwa na maneno haya: “Mwaminifu, mshikamanifu, hataruhusu nafsi yake iogope kamwe.”c Macho yetu sote yalijaa machozi!
-
-
Kwa Msaada wa Yehova, Tuliokoka Serikali za KimabavuMnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 1
-
-
c Ni wimbo namba 101 katika kitabu cha nyimbo cha 1928 chenye kichwa Nyimbo za Kumsifu Yehova, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Katika kitabu cha sasa cha nyimbo, ni wimbo namba 56.
-