-
Ni Nani Walio Watumwa Leo?Amkeni!—2000 | Machi 8
-
-
Ni Nani Walio Watumwa Leo?
HEBU wazia idadi yao. Inakadiriwa kwamba kati ya watoto milioni 200 na 250 wenye umri unaopungua miaka 15 hutumia muda mwingi wakati wa asubuhi kazini. Watoto robo milioni, wengine wakiwa na umri mchanga wa miaka saba, waliingizwa vitani mnamo mwaka wa 1995 na 1996 pekee, hivyo wengine wao wakawa watumwa wa vita. Idadi ya watoto na wanawake wanaouzwa wakiwa watumwa kila mwaka inakadiriwa kuwa zaidi ya milioni moja.
-
-
Ni Nani Walio Watumwa Leo?Amkeni!—2000 | Machi 8
-
-
Hali ya Utotoni Iliyoharibiwa
Katika kiwanda kimoja kidogo cha mikeka huko Asia, watoto wenye umri mdogo wa miaka mitano wanafanya kazi kuanzia saa kumi usiku hadi saa tano usiku bila malipo. Katika visa vingi watoto hao walioajiriwa hukabili hatari kubwa za kiafya: mashine zisizo salama, saa nyingi katika mazingira yasiyo na nuru na hewa ya kutosha, na kemikali hatari zinazotumiwa kutengeneza vitu.a
Kwa nini watoto hutafutwa kwa bidii ili wawe wafanyakazi? Kwa sababu ni rahisi kulipa watoto na kwa sababu kwa asili watoto hufundishika, ni rahisi kuwatia nidhamu, na huogopa kulalamika. Umbo lao dogo na vidole vyepesi huonwa na waajiri wasiozingatia kanuni zozote kuwa rasilimali ya kufanya aina fulani za kazi kama vile, kufuma mikeka. Mara nyingi watoto hao huajiriwa, huku wazazi wao wakikaa nyumbani, bila kazi ya kuajiriwa.
Jambo linalofanya hali ya watoto walioajiriwa kufanya kazi ya nyumbani iwe mbaya zaidi, hasa ni uwezekano wa kutendwa vibaya kingono na kimwili. Watoto wengi hutekwa nyara, huzuiwa kwenye kambi za mbali, na kufungiwa usiku ili kuwazuia wasitoroke. Huenda wakafanya kazi ya kujenga barabara na kuchimba mawe wakati wa mchana.
Njia nyingine ambayo hali ya utotoni huharibiwa ni kupitia ndoa ya kiutumwa. Shirika la Kimataifa Linalopinga Utumwa laeleza kisa kimoja cha mfano: “Msichana mwenye umri wa miaka 12 aambiwa kwamba familia yake imepanga afunge ndoa na mwanamume mwenye umri wa miaka 60. Ni wazi kwamba ana haki ya kukataa, lakini kihalisi hana fursa ya kudhihirisha haki hiyo na hana habari kwamba anaweza kufanya hivyo.”
-