Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Vitu Ambavyo Lazima Vitukie Karibuni
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Ufunuo kwa Yesu Kristo, ambao Mungu alimpa, aonyeshe watumwa wake vitu ambavyo lazima vitukie karibuni.” (Ufunuo 1:1a, NW) Kwa hiyo Yesu Kristo aliyefufuliwa ndiye aliyepokea ujumbe huu wenye maana kubwa kutoka kwa Mungu. Mbali na kuwa sehemu ya Utatu wa kifumbo, Yesu anaonyeshwa hapa kuwa akimtii Baba yake. Katika njia iyo hiyo, wale “watumwa” wanaofanyiza kundi la Kikristo wanamtii Yesu Kristo, hivi kwamba ‘huendelea kufuata yeye kokote aendako.’ (Ufunuo 14:4, NW; Waefeso 5:24) Lakini ni nani leo walio “watumwa” wa Mungu kikweli, nao Ufunuo unawanufaishaje?

      3. (a) Ni nani walio “watumwa” ambao wanamtii Yesu Kristo? (b) Ni kazi gani wanayofanya wale “watumwa” waaminifu chini ya mwelekezo wa kimalaika?

      3 Mtume Yohana, aliyeandika Ufunuo, anajieleza mwenyewe kuwa mmoja wa watumwa hao. Yeye ndiye aliyekuwa mtume wa mwisho kuishi na mmoja wa kile kikundi cha “watumwa” waliochaguliwa na kupakwa mafuta ambao wanarithi uhai usioweza kufa katika mbingu. Leo, kuna maelfu machache tu ya hawa yanayobaki duniani. Mungu ana watumishi wengine pia, kundi kubwa lao, wanaume, wanawake, na watoto, ambao sasa hesabu yao imefikia mamilioni. Chini ya mwelekezo wa kimalaika, hawa wanashiriki pamoja na “watumwa” wapakwa-mafuta katika kutangaza habari njema za milele kwa aina yote ya binadamu. Oh, jinsi “watumwa” wote hawa wanavyojitumikisha wenyewe ili kusaidia wapole wa dunia wapate wokovu! (Mathayo 24:14; Ufunuo 7:9, 14; 14:6) Ufunuo unaonyesha yale ambayo ni lazima wewe ufanye ili unufaishwe na habari njema zenye kuleta furaha.

  • Vitu Ambavyo Lazima Vitukie Karibuni
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 6. Yesu alitambulishaje ule mfereji ambao angetumia kuandalia ‘watumwa’ wake chakula cha kiroho leo?

      6 Mungu alikuwa na mfereji wa kuwasilisha Ufunuo katika siku ya Yohana, na Yohana alikuwa ndiye sehemu ya kidunia ya njia hiyo. Vivyo hivyo, Mungu ana njia ya kutolea ‘watumwa’ wake ulishaji wa kiroho leo. Katika unabii wake mkubwa kuhusu umalizio wa mfumo wa mambo, Yesu alitambulisha sehemu ya njia hii ya kidunia kuwa “mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu, ambaye, Bwana-mkubwa wake aliweka juu ya watu wake wa nyumba, kuwapa chakula chao kwa wakati unaofaa.” (Mathayo 24:3, 45-47, NW) Yeye anatumia jamii hii ya Yohana katika kufungua maana ya unabii huo.

  • Vitu Ambavyo Lazima Vitukie Karibuni
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Mfereji wa Mawasiliano

      5. Ufunuo uliwasilishwaje kwa mtume Yohana na kisha kwa makundi?

      5 Ufunuo 1:1b, 2, NW unaendelea kusema: “Na yeye [Yesu] alituma malaika wake na kuutoa [Ufunuo] kwa njia ya ishara kupitia yeye kwa mtumwa wake Yohana,

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki