Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Usingizi Ni Starehe Tu au Ni Muhimu?
    Amkeni!—2003 | Machi 22
    • Muda wa saa mbili hivi baada ya kulala usingizi, macho yetu huanza kusogea-sogea haraka. Jambo hilo limewafanya wanasayansi wagawanye usingizi katika vipindi viwili: kipindi cha kusogeza macho haraka na kipindi cha kutosogeza macho. Kipindi cha kutosogeza macho kinaweza kugawanywa katika vipindi vingine vinne vya usingizi mzito zaidi. Vipindi hivyo viwili hubadilishana mtu anapolala usingizi mzito.

      Mara nyingi, mtu huota ndoto wakati wa kipindi cha kusogeza macho. Pia misuli ya mwili hulegea kabisa, na hivyo mtu huamka akiwa mchangamfu. Isitoshe, watafiti fulani wanaamini kwamba habari mpya huhifadhiwa katika kumbukumbu letu la kudumu katika kipindi hicho cha usingizi.

      Wakati wa usingizi mzito (kipindi cha 3 na cha 4 cha kutosogeza macho), shinikizo letu la damu na mpigo wa moyo hupungua zaidi, na hivyo kupumzisha mzunguko wa damu na kumwepusha mtu na ugonjwa wa moyo. Zaidi ya hilo, homoni nyingi za ukuzi hutengenezwa wakati wa kipindi cha kutosogeza macho huku miili ya vijana fulani ikitengeneza homoni za ukuzi mara 50 zaidi wakati wa usiku kuliko mchana.

  • Usingizi Ni Starehe Tu au Ni Muhimu?
    Amkeni!—2003 | Machi 22
    • [Grafu katika ukurasa wa 5]

      (Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

      VIPINDI VYA USINGIZI

      Grafu sahili

      Vipindi vya Usingizi

      Kuwa macho

      Kipindi cha kusogeza macho haraka

      Kipindi cha kutosogeza macho

      Usingizi mwepesi 1

      2

      3

      Usingizi mzito 4

      1 2 3 4 5 6 7 8

      Saa za Usingizi

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki