-
Matokeo ya Jitihada za Kupambana na MagonjwaAmkeni!—2004 | Mei 22
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 8]
Kushinda Ndui na Polio
Mwishoni mwa Oktoba 1977, Shirika la Afya Ulimwenguni lilimpata mtu wa mwisho aliyekuwa akiugua ugonjwa wa ndui. Ali Maow Maalin, mpishi wa hospitali aliyekuwa akiishi Somalia, hakulemewa sana na ugonjwa huo, naye alipona baada ya majuma machache. Watu wote waliokuwa wameshirikiana naye walichanjwa.
Madaktari walisubiri kwa miaka miwili. Mtu yeyote ambaye angeripoti kisa kingine cha kweli cha mtu anayeugua ndui angepata zawadi ya dola 1,000. Hakuna yeyote aliyeripoti kisa cha kweli, na mnamo Mei 8, 1980, Shirika la Afya Ulimwenguni likatangaza rasmi kwamba “Ulimwengu na wakazi wake wote wameushinda ugonjwa wa ndui.” Miaka kumi tu iliyotangulia, ugonjwa wa ndui ulikuwa ukiua watu milioni mbili kila mwaka. Kwa mara ya kwanza katika historia, ugonjwa hatari wa kuambukiza ukawa umekomeshwa.a
-
-
Matokeo ya Jitihada za Kupambana na MagonjwaAmkeni!—2004 | Mei 22
-
-
a Ugonjwa wa ndui ulifaulu kukomeshwa ulimwenguni pote kupitia chanjo kwa sababu, tofauti na magonjwa mengine ambayo huenezwa vinginevyo kama vile kupitia panya na wadudu, virusi vya ndui huishi mwilini mwa binadamu tu.
-