-
Biblia Inabadili MaishaMnara wa Mlinzi—2009 | Agosti 1
-
-
Niliacha mara moja kuvuta bangi. Lakini ilinichukua miezi sita kuacha zoea la kuvuta tumbaku. Siku moja Shahidi aliyejifunza Biblia pamoja nami aliniuliza, “Una kusudi gani maishani?” Hilo lilinifanya nifikirie kwa uzito kuhusu zoea langu la kuvuta tumbaku. Nilikuwa nimejaribu mara nyingi kuacha kuvuta tumbaku. Hata hivyo, sasa niliamua kusali kabla ya kugusa sigareti badala ya kumwomba Mungu msamaha baadaye. Katika mwaka wa 1993, nilichagua siku moja ambayo ningeacha kuvuta. Kwa msaada wa Yehova, tangu wakati huo sijawahi tena kugusa sigareti.
-
-
Biblia Inabadili MaishaMnara wa Mlinzi—2009 | Agosti 1
-
-
Mara nyingi, nilimwomba Yehova anisaidie huku nikitokwa na machozi. Lakini ni wazi kwamba mwanzoni nilifanya mambo kwa njia isiyofaa, nilijiambia kwamba hii ndiyo mara yangu ya “mwisho” kabisa kuvuta sigareti kisha nilisali baada ya kuvuta. Shahidi aliyenifundisha Biblia alinisaidia kuona umuhimu wa kusali kabla ya kuchukua sigareti.
-