-
Shinda Vikwazo Vinavyokuzuia Usifanye Maendeleo!Mnara wa Mlinzi—2001 | Agosti 1
-
-
Au fikiria mwanamke aitwaye Keiko. Biblia ilimsaidia kuacha mazoea mabaya kama vile kuabudu sanamu, mwenendo mchafu, na uaguzi. Hata hivyo, Keiko anakiri: “Kikwazo kilichokuwa kikubwa zaidi kwangu ni kuvuta tumbaku. Nilijaribu mara nyingi kuacha lakini sikuweza.”
-
-
Shinda Vikwazo Vinavyokuzuia Usifanye Maendeleo!Mnara wa Mlinzi—2001 | Agosti 1
-
-
Vipi Keiko aliyekuwa na zoea la kuvuta tumbaku? Dada aliyekuwa anajifunza naye alipendekeza kwamba asome makala mbalimbali za Amkeni! kuhusu zoea hilo. Keiko hata aliweka maneno ya 2 Wakorintho 7:1 kwenye gari lake ili yawe yakimkumbusha kila siku kuwa safi machoni pa Yehova. Hata hivyo, hangeweza kuacha kuvuta tumbaku. “Jambo hilo liliniudhi sana,” Keiko akumbuka. “Ndipo nikaanza kujiuliza nilichotaka hasa—je, nilitaka kumtumikia Yehova au Shetani?” Alipoamua kwamba anataka kumtumikia Yehova, alisali kwa bidii apate msaada. “Nilishangaa kwamba niliweza kuacha kuvuta tumbaku bila shida. Ninajuta tu kwamba sikuacha mapema zaidi,” yeye anasema.
-