Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Waweza Kuacha—Sisi Tuliacha!”
    Amkeni!—1998 | Desemba 8
    • “TULITAKA tujihisi kuwa watu wazima, tuzifahamu hisia-moyo za utu mzima.”—Akio, Osamu, na Yoko.

      “Nilitaka kupunguza uzani.”—Tsuya.

      “Ulikuwa udadisi tu.”—Toshihiro.

      “Hatukufikiri kwamba tumbaku ingetuathiri vibaya.”—Ryohei, Junichi, na Yasuhiko.

      “Sikutaka nihisi vibaya kutokana na kichefuchefu nilipokuwa na mimba ya pili.”—Chieko.

      “Niliivuta ili nisione fedheha katika nyakati za kufedhehesha kwenye mikutano ya kikazi.”—Tatsuhiko.

  • “Waweza Kuacha—Sisi Tuliacha!”
    Amkeni!—1998 | Desemba 8
    • “Jinsi Tulivyoacha”

      Mieko: “Nilipoanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova, nilikuwa na uhakika kwamba singeweza kuacha kuvuta sigareti. Nia yangu ya kujifunza ilikuwa kwamba angalau watoto wangu wajifunze njia ya kupata uhai. Lakini punde si punde nikatambua kwamba lazima mzazi aweke kielelezo chema, kwa hiyo nikaanza kusali kwa bidii kwa Yehova Mungu anisaidie. Ilihitaji jitihada kufanyia kazi sala yangu, nami nilihisi vibaya sana kwa muda fulani. Lakini sitasahau kamwe hisia nzuri ajabu ya dhamiri safi ambayo niliiona hatimaye nilipoacha uovu huu mchafu.”

      Masayuki: “Baada ya kuwa mvutaji-sigareti wa pakiti tatu kwa siku na baada ya kujaribu sana na kushindwa, hatimaye nilizima sigareti yangu ya mwisho na kuacha tumbaku. Familia yangu, Mashahidi wenzangu, na Yehova Mungu walinisaidia kuacha. Katika benki ambako nilifanya kazi, hakuna aliyeamini kwamba nimeacha. Nilidokeza kwamba, kwa kuwaheshimu wateja wetu, wafanyakazi wa ofisi katika sehemu ya watu wote ya benki wasivute sigareti saa za kazi. Dokezo langu lilikubaliwa, hata ingawa asilimia 80 ya wafanyakazi walikuwa wavutaji-sigareti. Zoea hilo sasa limeenea katika matawi 260 ya benki yetu.”

      Osamu: “Nilipokuwa nikijifunza kweli ya Neno la Mungu, Biblia, nilijua ni lazima niache kuvuta sigareti. Ilinichukua mwaka mmoja hivi. Hata nilipoacha, kwa miezi sita mingine, ilinibidi nipigane na tamaa ya kuvuta sigareti. Nilijua moyoni mwangu kwamba ni lazima nitake kuacha.”

      Toshihiro: “Dhabihu ya fidia ya Yesu ilinivutia sana hivi kwamba nikahisi ningeweza angalau kujidhabihu kuacha kuvuta sigareti.”

      Yasuhiko: “Uamuzi wangu wa kumtii Yehova Mungu na kuacha kuvuta sigareti uliokoa uhai wangu. Siku moja, chumba ambacho nilikuwa nikifanyia kazi kilijaa gesi ya propani iliyokuwa ikivuja. Kwa kawaida, ningewasha sigareti, ambayo ingesababisha mlipuko. Lakini kwa kuwa nilikuwa nimeacha kuvuta sigareti siku chache kabla ya hapo, leo niko hai kuzungumzia jambo hilo.”

      Akio: “Nilipoanza kuhisi kichefuchefu mara kwa mara, nilikisia kwamba uvutaji-sigareti ulikuwa unaniumiza. Lakini sikuacha. Nilipata habari ya hakika ya kwanza kuhusu hatari za uvutaji-sigareti kwa mke wangu, ambaye alikuwa amekuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Upesi nikaanza kujifunza Biblia, nikajifunza kutokana na vichapo vya Watch Tower kwamba mvutaji-sigareti hajiumizi mwenyewe tu bali pia huumiza washiriki wa familia yake. Nikakoma mara moja!”

      Ryohei: “Mke wangu alikuwa akininunulia sigareti—pakiti 20 mara moja. Lakini baada ya kujifunza Biblia na Mashahidi, alikataa kununua kitu ambacho alijua kingenidhuru. Basi nikafungua duka langu mwenyewe la tumbaku. Nilikuwa nikivuta pakiti tatu na nusu kwa siku. Kisha nikaanza kujifunza Biblia na Mashahidi. Punde si punde nikataka kuwa msemaji mzuri wa habari za Biblia. Kwa hiyo, nikaacha kuvuta sigareti ili nistahili mazoezi haya katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.”

      Junichi: “Binti yangu mdogo ambaye ni Shahidi, alihangaikia maisha yangu. Alinifanya niahidi kuacha kuvuta sigareti, nikaacha.”

      Tsuya: “Nilipotembelea Jumba la Ufalme kwa mara ya kwanza, niliomba kisahani cha kuwekea jivu na kiberiti nilipokuwa nikiingia. Nilishangaa nilipoambiwa kwamba watu hawavuti sigareti huko. Nilijua ni lazima niache kuvuta sigareti. Siku nane nilizokaa hospitalini zilinisadikisha kwamba sikutaka kamwe kuhisi uchungu wa kuacha tena.”

      Yoko: “Nilijifunza jambo hilo katika magazeti na vichapo vingine vya Mashahidi wa Yehova, vikionyesha jinsi Yesu alivyokataa dawa za kulevya alizopewa wakati alipokuwa karibu kupigiliwa msumari kwenye mti wa mateso. Nilisali kwa Yehova Mungu, nikimwambia kwamba nataka kuwa msifaji safi wa jina lake. Baada ya hapo, sikuvuta sigareti tena. Watu waliokuwa karibu nami walipovuta sigareti, nilikuwa karibu kutaka kuvuta moshi wao, lakini niliondoka penye moshi haraka, kwa kuwa sikutaka hamu yangu ya kuvuta sigareti inirudie.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki