Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tunapaswa Kuwaonaje Watu Siku ya Yehova Inapokaribia?
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Julai 15
    • Abrahamu Alikuwa na Maoni ya Yehova

      3. Yehova aliwaonaje wakaaji wa Sodoma na Gomora?

      3 Mfano wa kwanza unahusu mzee wa ukoo Abrahamu, aliyekuwa mwaminifu, na miji yenye uovu ya Sodoma na Gomora. Yehova aliposikia “malalamiko mengi dhidi ya watu wa Sodoma na Gomora,” hakuharibu miji hiyo na wakaaji wake mara moja. Kwanza alifanya uchunguzi. (Mwanzo 18:20, 21, Biblia Habari Njema) Malaika wawili walitumwa Sodoma, ambako waliishi katika nyumba ya Loti, mwanamume mwenye haki. Usiku ambao malaika hao walifika, ‘watu wa mji waliizunguka nyumba, vijana kwa wazee, watu wote waliotoka pande zote,’ wakitaka kufanya ngono za wanaume kwa wanaume pamoja na malaika hao. Ni wazi kwamba, hali iliyopotoka ya wakaaji wa miji hiyo ilionyesha kwamba ilistahili kuharibiwa. Hata hivyo, malaika hao walimwambia Loti hivi: “Je! unaye mtu hapa zaidi? Mkwe, wanao, na binti zako, na wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa.” Yehova alifungua njia ili awaokoe baadhi ya wakaaji wa mji huo, lakini mwishowe, Loti tu na binti zake wawili ndio waliokoka uharibifu.—Mwanzo 19:4, 5, 12, 16, 23-26.

      4, 5. Kwa nini Abrahamu aliwaombea wakaaji wa Sodoma, na je, maoni yake kuhusu watu yalikuwa sawa na ya Yehova?

      4 Sasa, na turudi nyuma hadi wakati ambapo Yehova alifunua kusudi lake la kuichunguza miji ya Sodoma na Gomora. Wakati huo Abrahamu aliomba hivi: “Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu, wala hutauacha mji kwa ajili ya hao hamsini wenye haki waliomo? Hasha usifanye hivyo, ukamwue mwenye haki pamoja na mwovu, mwenye haki awe kama mwovu. Hasha; Mhukumu ulimwengu wote asitende haki?” Abrahamu alitumia neno “hasha” mara mbili. Kutokana na mambo aliyojionea, Abrahamu alijua kwamba Yehova hawezi kuharibu wenye haki pamoja na waovu. Yehova aliposema kwamba hangeharibu Sodoma kama kungekuwa na watu “wenye haki hamsini katika mji,” Abrahamu alipunguza hesabu hiyo hatua kwa hatua hadi ikafika watu kumi tu.—Mwanzo 18:22-33.

      5 Je, Yehova angesikiliza maombi ya Abrahamu kama yangekuwa kinyume cha maoni yake? La, hangemsikiliza. Akiwa “rafiki ya Yehova,” yaonekana Abrahamu alijua na alikubaliana na maoni Yake. (Yakobo 2:23) Wakati Yehova alipoelekeza fikira zake juu ya Sodoma na Gomora, alikuwa tayari kusikiliza maombi ya Abrahamu. Kwa nini? Kwa sababu Baba yetu wa mbinguni “hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.”

  • Tunapaswa Kuwaonaje Watu Siku ya Yehova Inapokaribia?
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Julai 15
    • Wewe Una Mtazamo Gani?

      11. Yaelekea Abrahamu angewaonaje watu wanaoishi leo?

      11 Leo, tunakaribia uharibifu mwingine wa mfumo huu mwovu wa mambo katika siku kuu ya Yehova. (Luka 17:26-30; Wagalatia 1:4; 2 Petro 3:10) Abrahamu angewaonaje watu wanaoishi katika ulimwengu huu ambao utaharibiwa karibuni? Yaelekea sana kwamba angewahangaikia watu ambao bado hawajasikia “habari njema hii ya ufalme.” (Mathayo 24:14) Abrahamu alimsihi Mungu tena na tena kuhusu watu fulani wa Sodoma ambao huenda walikuwa wenye haki. Je, sisi tunawahangaikia watu ambao wanaweza kuacha mienendo ya ulimwengu huu unaoongozwa na Shetani kama wangepewa nafasi ya kutubu na kumtumikia Mungu?—1 Yohana 5:19; Ufunuo 18:2-4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki