Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Mungu Ndiye Anayeikuza’!
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Julai 15
    • 7. Mbegu na udongo wa aina mbalimbali unawakilisha nini?

      7 Ona kwamba Yesu hasemi kwamba mbegu zinazopandwa ni za aina mbalimbali. Badala yake, anazungumzia mbegu ya aina moja ambayo inaanguka kwenye udongo wa aina mbalimbali, na kila moja inakuwa na matokeo tofauti. Udongo wa kwanza ni mgumu au umeshindiliwa; wa pili hauna kina; wa tatu umejaa miiba; na wa nne ni udongo mzuri na unatokeza mazao mengi. (Luka 8:8) Mbegu ni nini? Ni ujumbe wa Ufalme ulio katika Neno la Mungu. (Mt. 13:19) Udongo wa aina mbalimbali unawakilisha nini? Watu wenye mioyo yenye hali tofauti-tofauti.—Soma Luka 8:12, 15.

  • ‘Mungu Ndiye Anayeikuza’!
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Julai 15
    • Daraka la Wale Wanaosikiliza Neno

      10. Ni nini kinachoamua ikiwa mtu anayelisikia neno yuko kama udongo mzuri au mbaya?

      10 Namna gani wale wanaosikiliza neno? Je, imeamuliwa kimbele jinsi watakavyoitikia? Hapana. Ni juu yao kuchagua ikiwa watakuwa kama udongo mzuri au mbaya. Kwa kweli, hali ya moyo wa mtu inaweza kubadilika na kuwa nzuri au mbaya. (Rom. 6:17) Katika mfano wake, Yesu alisema kwamba “mara tu baada ya [wengine] kulisikia” lile neno, Shetani huja na kuliondoa. Lakini si lazima iwe hivyo. Katika Yakobo 4:7, Wakristo wanatiwa moyo ‘wampinge Ibilisi,’ kisha atawakimbia. Yesu alisema kwamba wengine wanalipokea neno kwa shangwe mwanzoni lakini baada ya muda wanakwazwa kwa sababu hawana “mzizi ndani yao wenyewe.” Lakini watumishi wa Mungu wanahimizwa ‘watie mizizi na kuimarishwa juu ya ule msingi’ ili waweze kufahamu akilini “upana na urefu na kimo na kina, na kuujua upendo wa Kristo ambao unazidi ujuzi.”—Efe. 3:17-19; Kol. 2:6, 7.

      11. Mtu anaweza kufanya nini ili mahangaiko na utajiri usilisonge lile neno?

      11 Yesu alisema kwamba wengine wanaolisikia neno wanaruhusu “mahangaiko ya mfumo huu wa mambo na nguvu za udanganyifu za utajiri” zipenye na kulisonga neno. (1 Tim. 6:9, 10) Wanaweza kuepuka jinsi gani hali hiyo? Mtume Paulo anajibu hivi: “Namna yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa, huku mkiridhika na vitu vya sasa. Kwa maana yeye amesema: ‘Sitakuacha wala kukutupa hata kidogo.’”—Ebr. 13:5.

      12. Kwa nini wale ambao ni kama udongo mzuri wanazaa matunda kwa viwango tofauti-tofauti?

      12 Mwishowe, Yesu anasema kwamba wale wanaopandwa kwenye udongo mzuri ‘wanazaa matunda 30 na 60 na 100.’ Hata ingawa watu fulani wanaolikubali neno wana hali nzuri ya moyo na wanazaa matunda, mambo ambayo wanatimiza wanapotangaza habari njema yanatofautiana kulingana na hali zao. Kwa mfano, uzee au ugonjwa wenye kudhoofisha unaweza kuwazuia wengine wasifanye mengi katika kazi ya kuhubiri. (Linganisha Marko 12:43, 44.) Vivyo hivyo, huenda mpandaji asiweze kubadili hali hizo, lakini anashangilia anapoona kwamba Yehova ameikuza.—Soma Zaburi 126:5, 6.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki