Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Amkeni!—2005 | Aprili 22
    • Maria alipoambiwa kwamba angepata mtoto na kumwita Yesu, aliuliza: “Hilo litawezekanaje, kwa kuwa silali na mwanamume?” Malaika Gabrieli aliyetumwa na Mungu akamjibu hivi: “Nguvu za Aliye Juu Zaidi zitakufunika. Kwa sababu hiyo pia kile kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.”—Luka 1:30-35.

      Baadaye, Yesu alifanya miujiza iliyowastaajabisha mitume wake. Dhoruba kali ilipotishia kupindua mashua yao kwenye Bahari ya Galilaya, Yesu aliyatuliza maji kwa kuyakemea: “Nyamaza, utulie!” Kwa mshangao, mitume wake wakauliza: “Kwa kweli huyu ni nani?”—Marko 4:35-41; Mathayo 8:23-27.

      Watu wengi walioishi siku zake, walitaka kujua Yesu ni nani, kwa hiyo, Yesu aliwauliza mitume wake watu wanasema yeye ni nani. “Baadhi yao husema Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, na wengine bado Yeremia au mmoja wa manabii.” Wote hao walikuwa tayari wamekufa. Kisha Yesu akawauliza: “‘Ninyi mnasema mimi ni nani?’ Simoni Petro akajibu, akasema: ‘Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.’” Hata mashetani—malaika waovu—walisema hivi kumhusu Yesu: “Wewe ndiye Mwana wa Mungu.”—Mathayo 16:13-16; Luka 4:41.

  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Amkeni!—2005 | Aprili 22
    • Badala ya kujitangaza mwenyewe kuwa Mwana wa Mungu, Yesu aliacha watu wafikie mkataa huo wao wenyewe. Na hata watu wengine mbali na mitume wake walifikia mkataa huohuo, kutia ndani Yohana Mbatizaji na Martha, rafiki ya Yesu. (Yohana 1:29-34; 11:27) Watu hao waliamini kwamba Yesu ndiye Masihi aliyeahidiwa. Walijua kwamba aliishi mbinguni akiwa mtu wa kiroho mwenye nguvu na kwamba Mungu aliuhamisha uhai wake kimuujiza hadi kwenye tumbo la bikira Maria.—Isaya 7:14; Mathayo 1:20-23.

      Alilingana na Mtu wa Kwanza, Adamu

      Yesu alilingana sana na mwanadamu wa kwanza, Adamu. Kwa mfano, wote wawili walikuwa wanadamu wakamilifu wasio na baba wa kibinadamu. (Mwanzo 2:7, 15) Kwa hiyo, Biblia inamwita Yesu “Adamu wa mwisho”—mwanadamu mkamilifu ambaye angeweza kuwa “fidia inayolingana.” Maisha ya Yesu yalilingana na ya “mtu wa kwanza Adamu,” ambaye Mungu alimuumba akiwa mkamilifu.—1 Wakorintho 15:45; 1 Timotheo 2:5, 6.

      Katika Biblia, Adamu wa kwanza anaitwa “mwana wa Mungu.” (Luka 3:38) Hata hivyo, alipomwasi Mungu kimakusudi, Adamu huyo wa kwanza alipoteza uhusiano wake wenye thamani wa kuwa mwana wa Mungu. Kwa upande mwingine, sikuzote Yesu alikuwa mwaminifu kwa Baba yake wa mbinguni naye aliendelea kuwa Mwana wa Mungu anayekubalika. (Mathayo 3:17; 17:5)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki