-
Yehova Huleta Wana Wengi Kwenye UtukufuMnara wa Mlinzi—1998 | Februari 15
-
-
4 Yehova alitumia roho yake takatifu, au kani ya utendaji, kumzaa Yesu akiwa Mwana wake wa kiroho, ili amlete kwenye utukufu wa kimbingu. Alipokuwa peke yake pamoja na Yohana Mbatizaji, Yesu alizamishwa kabisa katika maji akionyesha kujitoa kwake kwa Mungu. Simulizi la Gospeli ya Luka lasema hivi: “Watu wote walipokuwa wamebatizwa, Yesu pia akabatizwa na, alipokuwa akisali, mbingu ilifunguliwa na roho takatifu katika umbo la kiwiliwili kama njiwa ikateremka juu yake, na sauti ikaja kutoka mbinguni: ‘Wewe ni Mwana wangu, mpendwa; nimekukubali wewe.’” (Luka 3:21, 22) Yohana aliona roho takatifu ikimjia Yesu na kumsikia Yehova akisema kwa kumkubali waziwazi kuwa Mwana Wake mpendwa. Wakati huo na kupitia roho takatifu, Yehova alimzaa Yesu akiwa wa kwanza wa ‘wana wengi ambao wataletwa kwenye utukufu.’
-
-
Yehova Huleta Wana Wengi Kwenye UtukufuMnara wa Mlinzi—1998 | Februari 15
-
-
7 Yesu alikuwa Mwana wa Mungu tangu kuzaliwa kwake kwa kibinadamu, kama vile mwanadamu mkamilifu Adamu alivyokuwa “mwana wa Mungu.” (Luka 1:35; 3:38) Hata hivyo, baada ya kubatizwa kwa Yesu, lilikuwa jambo la maana kwamba Yehova alijulisha wazi hivi: “Wewe ni Mwana wangu, mpendwa; nimekukubali wewe.” (Marko 1:11) Kupitia julisho hilo lenye kuandamana na mtiririko wa roho takatifu, ilikuwa wazi kwamba Mungu alimzaa Yesu wakati huo akiwa Mwana Wake wa kiroho. Kitamathali, wakati huo Yesu alipewa “uzaliwa mpya” pamoja na haki ya kupokea uhai mara nyingine tena akiwa Mwana wa Mungu aliye roho mbinguni.
-