-
Je, Una Nafsi Isiyoweza Kufa?Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 15
-
-
Neno “nafsi” linatumiwa katika maana nyingine pia. Katika Ayubu 33:22, tunasoma hivi: “Nafsi yake inakaribia shimoni, na uhai wake unakaribia waangamizi.” (Union Version) Hapa, maneno “nafsi” na “uhai” yanatumiwa kumaanisha kitu kimoja, na neno “nafsi” linapanua maana ya neno “uhai.” Kwa hiyo, neno “nafsi” linaweza pia kumaanisha uhai wa mtu, akiwa nafsi hai. Hivyo, Maandiko yanasema hivi kuhusu maadui wa Musa waliotaka kumuua: ‘Watu wote waliokuwa wakiiwinda nafsi yake wamekufa.’ (Kutoka 4:19) Na kumhusu Yesu Kristo, Biblia inasema hivi: ‘Mwana wa binadamu alikuja, kutoa nafsi yake, yaani, uhai wake kuwa fidia badala ya wengi.’—Mathayo 20:28.
-
-
Je, Una Nafsi Isiyoweza Kufa?Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 15
-
-
Lakini namna gani mistari ya Biblia inayosema kuhusu kutoka na kurudi kwa nafsi? Biblia inasema hivi kuhusu kile kilichompata Raheli alipomzaa mwana: “Nafsi yake ilipokuwa ikitoka (kwa sababu alikufa) akamwita jina lake Ben-oni; lakini baba yake akamwita Benyamini.” (Mwanzo 35:18) Na kuhusu ufufuo wa mwana wa mjane, 1 Wafalme 17:22 linasema: “Yehova akaisikiliza sauti ya Eliya [katika sala], hivi kwamba nafsi ya yule mtoto ikarudi ndani yake, akawa hai.” Je, mistari hiyo inaonyesha kwamba nafsi ni kitu fulani kisichoonekana, kisichoweza kuguswa, ambacho kinaondoka au kuingia mwilini?
Kumbuka kwamba maana moja ya neno “nafsi” ni “uhai.” Hivyo, nafsi ya Raheli ilikuwa ikitoka katika maana ya kwamba uhai wake ulikuwa ukifikia mwisho wake. Kwa kweli, katika Biblia fulani maneno “nafsi yake ilipokuwa ikitoka” yametafsiriwa hivi, “uhai wake ulipokuwa unafifia” (Knox) na “alipokuwa akivuta pumzi yake ya mwisho” (Jerusalem Bible). Vivyo hivyo, katika kisa cha mwana wa mjane, uhai ndio uliomrudia mtoto huyo.—1 Wafalme 17:23.
-