-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Andrew Masondo aliwekwa rasmi kuwa mwangalizi wa mzunguko mwaka wa 1954. Alisema: “Mwaka wa 1965, nilipewa mgawo wa kwenda Botswana, nao ulikuwa kama mgawo wa umishonari. Kulikuwa na njaa nchini humo kwa kuwa mvua haikuwa imenyesha huko kwa miaka mitatu. Mara nyingi mimi na mke wangu Georgina tulilala bila chakula cha jioni na kwenda shambani asubuhi bila kiamsha-kinywa. Kwa kawaida tulipata mlo mmoja tu, mchana.
“Niliporudi Afrika Kusini, niliwekwa rasmi kuwa mwangalizi wa wilaya nami nikazoezwa na Ernest Pandachuk. Maneno ya mwisho aliyoniambia yalikuwa, ‘Usiinue kamwe kichwa chako kuwapita akina ndugu, bali uwe kama mabua ya nafaka yanayoinamisha kichwa yanapoiva, na kuonyesha kwamba yana mazao tele.’”
-
-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 99]
Andrew Masondo na mke wake wa pili, Ivy
-