-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ivan Pashkovsky, mshiriki wa Halmashauri ya Nchi kwa zaidi ya miaka 30, anakumbuka hivi:
-
-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
KONDOO WANAISIKIA SAUTI YA MCHUNGAJI WAO
Halmashauri ya Nchi ilijitahidi sana kuwaunganisha akina ndugu. Chini ya hali zilizokuwepo, hilo halikuwa jambo rahisi. Kufikia kiangazi cha 1962, wilaya nzima ilikuwa imeunganishwa na tengenezo. Akina ndugu waliokomaa kiroho waliwekwa rasmi kuwa washiriki wa halmashauri ya pekee. Yehova alibariki jitihada za akina ndugu hao na akawapa “hekima inayotoka juu.” (Yak. 3:17) Aleksey Gaburyak, aliyekuwa mwangalizi wa mzunguko kuanzia 1986 mpaka 1995, anakumbuka hivi: “Tulikutana na washiriki wa Halmashauri ya Nchi huko Usol’ye-Sibirskoye mwaka wa 1965. Ndugu hao walituomba tuwatafute ndugu na dada wote waliokuwa wametawanyika kwa sababu ya kuhamishwa, kufungwa gerezani, au kwa sababu ya mgawanyiko uliokuwepo na kuwaunganisha tena na makutaniko. Tulipewa anwani kadhaa. Eneo langu lilitia ndani wilaya ya Tomsk na Kemerovo na pia majiji ya Novokuznetsk na Novosibirsk. Ndugu wengine walipewa maeneo tofauti. Tulipaswa kupanga makutaniko na vikundi mbalimbali na pia kuwaweka rasmi na kuwazoeza ndugu wanaostahili. Isitoshe, tulihitaji kupanga jinsi ambavyo vichapo vingewafikia akina ndugu na kupanga mikutano ya kutaniko chini ya marufuku. Kwa muda mfupi tu, tulifanikiwa kuwatembelea ndugu na dada 84 ambao walikuwa wametenganishwa na tengenezo. Jinsi tulivyofurahi kuona kwamba ‘kondoo’ wa Yehova walisikia tena sauti ya Mchungaji Mwema na walimtumikia pamoja na watu wake!”—Yoh. 10:16.
Muda si muda wengi waliokuwa wametenganishwa na tengenezo walijiunga tena na Halmashauri ya Nchi na wakaanza kutuma ripoti zao za utumishi wa shambani. Kufikia mwaka wa 1971, zaidi ya wahubiri 4,500 walikuwa wamejiunga tena na tengenezo la Yehova. Licha ya marufuku iliyokuwepo, kufikia miaka ya katikati ya 1980, kazi ya kuhubiri ilikuwa ikiendelea na wapya walikuwa wakiongezeka katika makutaniko.
-