-
Shabaha ya Mashambulizi ya SovietiAmkeni!—2001 | Aprili 22
-
-
Jitihada za Kukabiliana na Ongezeko
Viongozi wa Sovieti walijaribu mbinu mbalimbali ili kukomesha kazi ya Mashahidi wa Yehova. Walianzisha mpango madhubuti wa kueneza habari za uwongo kuhusu Mashahidi, kwa kuwa mnyanyaso mkali haukufaulu. Walitumia vitabu, filamu, na vipindi vya redio. Wapelelezi waliozoezwa wa KGB walijiunga na makutaniko kisirisiri.
Habari za uwongo zilizoenezwa kote ziliwafanya watu wengi wahofu na kutowaamini Mashahidi bila sababu, hilo lathibitishwa na makala moja katika kitabu Reader’s Digest cha Agosti 1982, Chapa ya Kanada. Makala hiyo iliandikwa na Vladimir Bukovsky, Mrusi aliyeruhusiwa kuhamia Uingereza mwaka wa 1976. Aliandika hivi: “Jioni moja niliona ubao kwenye jengo moja jijini London uliotangaza hivi: MASHAHIDI WA YEHOVA . . . Sikuweza kuendelea kusoma, nilipigwa na bumbuazi na kushtuka sana.”
Vladimir aeleza kilichomfanya ahofu: “Haya ndiyo madhehebu ambayo wenye mamlaka nchini mwetu huita mahayawani katili ili kuwaogopesha watoto . . . Katika Muungano wa Sovieti, ‘Mashahidi’ wako gerezani na kwenye kambi za mateso tu. Na sasa nilisimama mbele ya jengo na kutazama ubao wenye jina lao. Je, kweli mtu yeyote angeweza kuwatembelea tu kirafiki?” akauliza. Ili kukazia sababu iliyomfanya ahofu, Vladimir alimalizia kwa kusema hivi: “‘Mashahidi’ wanasakwa sana katika nchi yetu kama vile wahuni wa Mafia wanavyosakwa Uingereza, nao hawaeleweki hata kidogo.”
Lakini Mashahidi walivumilia na kuongezeka sana licha ya mnyanyaso mkali na uenezaji wa habari za uwongo kuwahusu. Vitabu vya Sovieti kama vile The Truths About Jehovah’s Witnesses, kilichochapishwa kwa nakala 100,000 za Kirusi, katika mwaka wa 1978, kilidokeza kwamba habari za uwongo zinazokashifu Mashahidi zinahitaji kuenezwa kwa mapana na marefu. Mtungaji wa kitabu hicho, V. V. Konik, ambaye alieleza jinsi Mashahidi walivyokuwa wakihubiri wajapozuiwa, alishauri hivi: “Wasovieti wanaochunguza dini wanapaswa kubuni njia bora zaidi za kukomesha mafundisho ya mashahidi wa Yehova.”
-
-
Shabaha ya Mashambulizi ya SovietiAmkeni!—2001 | Aprili 22
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 8]
ARMAGEDDON Filamu ya Sovieti Iliyoeneza Uwongo
Serikali ya Sovieti ilitayarisha filamu ya Armageddon ili kuharibu sifa ya Mashahidi wa Yehova. Ilikuwa hadithi ya kubuniwa ya mapenzi kati ya mvulana mmoja wa jeshi la Sovieti na msichana aliyeshawishiwa kuwa Shahidi. Mwishoni mwa filamu hiyo, dada mchanga wa msichana huyo alikufa katika aksidenti iliyosababishwa na mwangalizi mmoja Shahidi, ambaye alionyeshwa kuwa kibaraka wa shirika la upelelezi la Marekani.
Gazeti The Red Flag la Ukrainia la Mei 14, 1963 lilisema hivi kuhusu filamu hiyo iliyowaudhi watu: “Hivyo ndivyo wale wasiomwamini Mungu wanavyoeneza kwa matokeo habari za uwongo zinazosadikisha. Filamu hiyo inaweza kuonyeshwa katika vijiji vingine nchini.”
-