Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Urusi
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Ili kuwasaidia wote wawe imara kiroho, akina ndugu waliamua kufanya mikutano saba kwa juma. Mwanzoni kulikuwa na Biblia moja iliyokuwa ikitumiwa na makutaniko yote, hivyo kulikuwa na ratiba ya kusoma Biblia hiyo kutaniko moja hadi lingine. Nafasi ilipojitokeza, ndugu walinakili Biblia. Vitabu tofautitofauti vya Biblia vilinakiliwa kwenye madaftari na nakala halisi ya Biblia ilifichwa. Kwa njia hiyo akina ndugu waliweza kufuata ratiba iliyopangwa ya usomaji wa Biblia. Funzo la Mnara wa Mlinzi lilipangwa pia.

  • Urusi
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Mnamo 1958, kwenye kambi huko Mordvinia, akina ndugu walikuwa wakiongoza mikutano kwa ukawaida. Ili wanyapara wasiwakamate, ndugu kadhaa waliwekwa wasimame kila baada ya hatua chache ili watoe onyo wengine walipokuwa wakijifunza Mnara wa Mlinzi. Mnyapara alipotokea ndugu aliyemwona angesema “anakuja,” kisha ujumbe huo ungepitishwa hadi kwa kikundi kilichokuwa kimekutana. Kila mtu angeondoka, na gazeti lingefichwa. Lakini mara nyingi wanyapara walitokea ghafula na bila kutarajiwa.

      Wakati mmoja wanyapara walipowakuta ghafula akina ndugu, Boris Kryltsov aliamua kuwakengeusha ili wasilipate gazeti hilo. Alinyakua kitabu na kukimbia nje ya jengo. Wanyapara walimkimbiza kwa muda mrefu, lakini walipomkamata waliona alikuwa amebeba kitabu cha Lenin. Ingawa alitiwa katika kifungo cha upweke kwa siku saba, alifurahi kwamba alikuwa amesaidia gazeti lisichukuliwe.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki