-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Viktor Gutshmidt anakumbuka: “Wakati mmoja niliporudi nyumbani baada ya utumishi, nyumba yote ilikuwa imevurugwa. Maofisa wa KGB walikuwa wakitafuta vichapo. Walinikamata na kunihoji kwa miezi miwili. Yulia, binti yetu mdogo alikuwa na miezi 11, na binti yetu mkubwa alikuwa na miaka 2.
“Inspekta aliniambia hivi aliponihoji, ‘Wewe ni Mjerumani, sivyo?’ Watu wengi waliona neno ‘Mjerumani’ kuwa linarejezea ‘Mfashisti.’ Wajerumani walichukiwa.
“‘Mimi sitetei taifa langu,’ nilisema, ‘lakini ikiwa unauliza kuhusu Wajerumani niliofungwa nao kwenye kambi za mateso za Wanazi, basi ninawaheshimu Wajerumani hao kwelikweli! Waliitwa Bibelforscher, na sasa wanaitwa Mashahidi wa Yehova. Najivunia kwamba hakuna Shahidi aliyewahi kutumia bunduki ya kumimina risasi au kulipua kombora. Ninajivunia sana Wajerumani hao!’
“Inspekta huyo alinyamaza, kwa hiyo nikasema: ‘Nina hakika kwamba hakuna Shahidi wa Yehova ameshiriki katika uasi wowote. Hata kazi ya Mashahidi wa Yehova inapopigwa marufuku, wao huendelea kumwabudu Mungu. Wakati huohuo, Mashahidi hutambua na kutii mamlaka zinazofaa ikiwa sheria zao hazivunji sheria za juu zaidi za Muumba wetu.’
“Ghafula, inspekta huyo alinikatiza na kusema: ‘Hatujawahi kukichunguza kikundi kingine kwa uangalifu kama tulivyowachunguza Mashahidi na utendaji wao. Ikiwa rekodi zingeonyesha jambo lolote dhidi yenu, hata ikiwa ingepatikana kwamba mlimuumiza mtu mmoja tu, tungewapiga ninyi nyote risasi.’
“Kisha nikajiambia hivi: ‘Ndugu zetu ulimwenguni pote wana ujasiri wa kumtumikia Yehova, na mfano wao umetuokoa huku katika Muungano wa Sovieti. Kwa hiyo, huenda kumtumikia Mungu hapa kukawasaidia ndugu zetu katika maeneo mengine.’ Wazo hilo lilinipa nguvu za kushikamana na njia za Yehova.”
-
-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 110]
Viktor Gutshmidt
-