Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mfalme Atafuta Hekima
    Amkeni!—2007 | Januari
    • Biblia Alfonsina

      Ujuzi ambao wasomi hao wa Toledo walipata kwa kutafsiri vichapo vingi uliwasaidia Alfonso alipowaamuru watafsiri sehemu za Biblia kwa Kihispania. Kulingana na mwanahistoria Mhispania, Juan de Mariana, mfalme alitoa pesa ili Biblia hiyo itafsiriwe akitumaini kuwa kufanya hivyo kutaboresha lugha ya Kihispania. Bila shaka, tafsiri hizo za awali za Biblia zilichangia kuendeleza lugha ya Kihispania.

      Mfalme aliiona Biblia kuwa yenye thamani kwa ajili ya kuwafundisha wanadamu. Aliandika hivi katika utangulizi wa kitabu Crónica de España: “Tukichunguza manufaa yanayotokana na Maandiko Matakatifu, tunaona kuwa kuna mafundisho tunayopata kuhusu kuumbwa kwa ulimwengu, kuja kwa baba wa ukoo, . . . kuja kulikoahidiwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo, kuteswa, kufufuliwa, na kupaa kwake mbinguni.”

      Pia alikagua matayarisho ya vichapo vya fasihi alivyoiita General Estoria. Vilitia ndani kutafsiriwa kwa sehemu fulani za Maandiko ya Kiebrania katika Kihispania. (Sehemu fulani za Maandiko ya Kigiriki zilitafsiriwa baadaye.) Biblia hiyo ya kupendeza, inayojulikana kama Biblia Alfonsina, ndiyo iliyokuwa kubwa zaidi kutokezwa katika Enzi za Kati. Ilinakiliwa mara nyingi na sehemu fulani zilitafsiriwa katika Kireno na sehemu nyingine kwa Kikatalani.

  • Mfalme Atafuta Hekima
    Amkeni!—2007 | Januari
    • [Picha katika ukurasa wa 13]

      Mfalme akiwa pamoja na watafsiri kutoka Toledo (juu); akiwa na wachoraji (chini); Injili ya Luka katika “Biblia Alfonsina” (chini kabisa)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki