Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tauni Mbaya Zaidi Katika Historia
    Amkeni!—2005 | Desemba 22
    • Ugonjwa Usio wa Kawaida

      Tofauti kubwa kati ya homa hiyo na nyingine ni kwamba iliua haraka. Iliua haraka kadiri gani? Katika kitabu cha karibuni kinachoitwa The Great Influenza, mwandikaji John M. Barry ananukuu visa fulani kuhusu ugonjwa huo: “Huko Rio de Janeiro, mwanamume fulani alimwuliza Ciro Viera Da Cunha, aliyekuwa akisomea udaktari, habari fulani kwa sauti ya kawaida kabisa walipokuwa wakingojea tramu, kisha akaanguka na kufa; huko Cape Town, Afrika Kusini, Charles Lewis alipanda tramu kuelekea nyumbani kwake umbali wa kilometa tano wakati kondakta alipoanguka na kufa. Gari hilo liliposafiri kilometa tano zilizosalia, watu wengine sita kutia ndani dereva walikufa.” Wote walikufa kutokana na homa hiyo.

  • Tauni Mbaya Zaidi Katika Historia
    Amkeni!—2005 | Desemba 22
    • Pia, watu waliogopa kwa sababu homa hiyo iliwapata watu bila kubagua. Kwa sababu ambazo bado hazieleweki, ugonjwa huo wa mwaka wa 1919 haukuwapata tu wazee; uliwapata na kuwaua vijana wenye afya. Wengi wa waliokufa kutokana na homa ya Hispania walikuwa na umri wa kati ya miaka 20 na 40.

      Isitoshe, tauni hiyo ilienea ulimwenguni pote. Hata ilifika kwenye visiwa vya tropiki. Homa hiyo ilipelekwa Samoa Magharibi (sasa inaitwa Samoa) na meli Novemba 7, 1918, na baada ya miezi miwili, asilimia 20 hivi ya wakazi 38,302 wa huko walikufa. Nchi zote kubwa za ulimwengu ziliathiriwa sana!

      Pia, tauni hiyo iliua watu wengi sana. Kwa mfano, ugonjwa huo ulitokea mapema na kuua watu wengi sana huko Philadelphia, Pennsylvania, Marekani. Kufikia katikati ya Oktoba 1918, kulikuwa na upungufu mkubwa sana wa majeneza. “Mtengenezaji mmoja alisema kwamba angeweza kuuza majeneza 5,000 kwa muda wa saa mbili ikiwa angekuwa nayo. Nyakati nyingine chumba cha kuhifadhia maiti cha jiji kilikuwa na maiti zilizozidi idadi ya majeneza mara kumi,” anasema mwanahistoria Alfred W. Crosby.

      Baada ya muda mfupi tu, homa hiyo ilikuwa imeua watu wengi zaidi kuliko tauni yoyote iliyowahi kutokea katika historia ya wanadamu. Makadirio ya kawaida yanaonyesha kwamba watu milioni 21 walikufa ulimwenguni pote, lakini sasa wataalamu fulani wanasema kwamba idadi hiyo ni ndogo. Leo wataalamu fulani wa magonjwa ya kuambukiza wanadokeza kwamba huenda watu milioni 50 walikufa au labda milioni 100 hivi! Barry aliyetajwa juu anasema hivi: “Homa hiyo iliua watu wengi zaidi kwa mwaka mmoja kuliko wale waliouawa na Tauni iliyotokea Zama za Kati katika karne moja; iliua watu wengi zaidi katika majuma 24 kuliko wale ambao wameuawa na UKIMWI katika miaka 24.”

      Jambo la ajabu ni kwamba homa ya Hispania iliwaua Wamarekani wengi zaidi kwa mwaka mmoja hivi kuliko jumla ya waliokufa katika vita viwili vya ulimwengu. Mwandishi Gina Kolata anaeleza hivi: “Ikiwa tauni hiyo ingetokea leo, na kuua asilimia kama hiyohiyo ya Wamarekani, basi Wamarekani milioni 1.5 wangekufa. Idadi hiyo inazidi idadi ya wale wanaokufa kwa mwaka mmoja kutokana na ugonjwa wa moyo, kansa, kiharusi, magonjwa mabaya ya mapafu, UKIMWI, na ugonjwa wa Alzheimer yakijumlishwa.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki