-
Uwe na Maoni Yanayopatana na Maandiko Kuhusu MatibabuMnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
-
-
Mbinu fulani za kupima magonjwa na za matibabu zinatia ndani uchawi. Yehova aliwashutumu Waisraeli waasi-imani ambao walitumia “nguvu za uchawi,” au mazoea ya kuwasiliana na pepo. Alitangaza hivi: “Acheni kuleta ndani matoleo zaidi ya nafaka yasiyo na thamani. Uvumba—ni chukizo kwangu. Mwezi mpya na sabato, kuita mkusanyiko—siwezi kuvumilia matumizi ya nguvu za uchawi pamoja na kusanyiko kuu.” (Isa. 1:13) Bila shaka, ugonjwa si sababu ya kufanya jambo ambalo linaweza kuzuia sala zetu na kuharibu uhusiano wetu pamoja na Mungu.—Omb. 3:44.
-
-
Uwe na Maoni Yanayopatana na Maandiko Kuhusu MatibabuMnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
-
-
13, 14. (a) Shetani anaweza kuvunja utimilifu wetu jinsi gani kupitia matibabu tunayochagua? (b) Kwa nini tunapaswa kuepuka kitu chochote ambacho kinahusiana hata kwa kadiri ndogo na zoea la kuwasiliana na pepo?
13 Shetani atatumia njia yoyote ili kutufanya tuiache ibada ya kweli. Kama vile anavyotumia upotovu wa maadili katika ngono na tamaa ya vitu vya kimwili ili kuwaangusha watu fulani, ndivyo anavyojaribu kuvunja utimilifu wa wengine kupitia matibabu yasiyofaa ambayo yanatia ndani nguvu za uchawi na kuwasiliana na pepo. Tunasali ili Yehova atukomboe kutoka kwa “yule mwovu” na kutoka katika “kila namna ya uasi-sheria.” Kwa hivyo, hatupaswi kumpa Shetani nafasi ya kutunasa kwa kujihusisha na jambo lolote ambalo linatia ndani kuwasiliana na pepo na uchawi.—Mt. 6:13; Tito 2:14.
14 Yehova aliwakataza Waisraeli wasifanye uaguzi na uchawi. (Kum. 18:10-12) Paulo anasema kwamba “mazoea ya kuwasiliana na pepo” ni kati ya “matendo ya mwili.” (Gal. 5:19, 20) Kwa kuongezea, “wale wanaozoea kuwasiliana na pepo” hawataingia katika mfumo mpya wa mambo wa Yehova. (Ufu. 21:8) Basi, ni wazi kwamba kitu chochote ambacho kinahusiana hata kwa kadiri ndogo na zoea la kuwasiliana na pepo kinamchukiza Yehova.
“Usawaziko Wenu na Ujulikane”
15, 16. Kwa nini tunahitaji kuchagua matibabu kwa hekima, na baraza linaloongoza la karne ya kwanza lilitoa mashauri gani yenye hekima?
15 Kwa hivyo, ikiwa tuna shaka kuhusu matibabu fulani au njia yoyote ya kupima magonjwa, ni jambo la hekima kuikataa. Hata hivyo, hilo halimaanishi kwamba ikiwa hatuelewi matibabu fulani basi yanatia ndani zoea la kuwasiliana na pepo. Ili tuwe na maoni yanayopatana na Maandiko kuhusu matibabu, tunahitaji utambuzi na vilevile hekima inayotegemea Neno la Mungu. Tunahimizwa hivi katika Methali sura ya 3: “Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Mtambue yeye katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako. . . . Linda hekima inayotumika na uwezo wa kufikiri, nazo zitakuwa uzima kwa nafsi yako.”—Met. 3:5, 6, 21, 22.
-