Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Katika utimizo wake mkubwa, Isaya sura ya 62 inatuhakikishia kwamba wokovu wa taifa la kiroho la Yehova, yule “Israeli wa Mungu,” ni hakika.—Wagalatia 6:16.

  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • “Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia [“sitakaa kimya,” “NW”], hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo [“mwenge,” “VB”].”—Isaya 62:1.

  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Kwa karne nyingi, Jumuiya ya Wakristo ikawa imeruhusiwa kuleta suto kubwa juu ya jina la Yehova. Hata hivyo, mwishowe “mwaka wa nia njema” wa Yehova ukaanza katika mwaka wa 1914, pamoja na utimizo mkubwa wa sehemu hii ya unabii wa Isaya.—Isaya 61:2, NW.

      4, 5. (a) Sayuni na watoto wake wanafananisha nani leo? (b) Yehova ametumiaje Sayuni ili kufanya ‘wokovu wake uwe kama taa iwakayo’?

      4 Leo ahadi ya Yehova ya kurudisha Sayuni imetimizwa kuhusiana na tengenezo lake la kimbingu, “Yerusalemu la juu,” kama vile linavyowakilishwa duniani na watoto wake, Wakristo waliotiwa mafuta kwa roho. (Wagalatia 4:26) Tengenezo la Yehova la kimbingu ni msaidiaji mwenye moyo wa kujitoa—ni mlinzi aliye macho, mwenye upendo, na mwenye bidii. Mwaka wa 1914 ulikuwa pindi ya kusisimua kama nini wakati tengenezo hilo lilipozaa Ufalme wa Kimesiya! (Ufunuo 12:1-5) Kuanzia 1919 hasa, watoto wake wa kidunia wamehubiria mataifa kuhusu haki na wokovu wa tengenezo hilo. Kama vile Isaya alivyotabiri, watoto hawa wamelimulika giza kama mwenge, wakiacha nuru yao ing’ae.—Mathayo 5:15, 16; Wafilipi 2:15.

      5 Yehova anapendezwa sana na waabudu wake na hatapumzika, wala kukaa kimya, mpaka atimize ahadi zote alizomtolea Sayuni na watoto wake. Hata mabaki ya watiwa-mafuta pamoja na waandamani wao walio “kondoo wengine” wanakataa kukaa kimya. (Yohana 10:16) Wanatoa sauti kweli kweli wakiwaonyesha watu njia pekee ya kupata wokovu.—Waroma 10:10.

      Wapewa “Jina Jipya” na Yehova

      6. Yehova ana lengo gani kuhusu Sayuni?

      6 Yehova ana lengo gani kuhusu Sayuni, “mwanamke” wake wa kimbingu, aliyewakilishwa na Yerusalemu la kale? Anasema hivi: “Mataifa wataiona haki yako [“Ee mwanamke,” “NW”], na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha BWANA.” (Isaya 62:2)

  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Leo, Israeli wa Mungu wanasisimuka kuwa kipenzi cha Yehova kwa njia hiyo, na wale kondoo wengine wanashangilia pamoja nao.

      8. Yehova amemheshimu Sayuni kwa njia zipi?

      8 Akiisha kumpa Sayuni jina jipya, sasa Yehova anaahidi hivi: “Utakuwa taji ya uzuri katika mkono wa BWANA, na kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako.” (Isaya 62:3) Yehova anamwinua mke wake wa mfano, Sayuni wa kimbingu, atazamwe kwa mshangao kwa sababu anavutia. (Zaburi 48:2; 50:2) Taji la uzuri na “kilemba cha kifalme” zinaonyesha kwamba mke huyo amevikwa heshima na mamlaka. (Zekaria 9:16) Israeli wa Mungu, ambaye anawakilisha Sayuni wa kimbingu, au “Yerusalemu la juu,” ametokea kwa kufanyizwa vizuri ajabu na mkono wa Mungu, yaani nguvu zake zikiwa katika hali ya kutumika. (Wagalatia 4:26) Kwa msaada wa Yehova, taifa hilo la kiroho limeweka kumbukumbu zuri ajabu la uaminifu wa maadili na moyo wa kujitoa kwa muda mrefu. Mamilioni ya watu, kutia na watiwa-mafuta na kondoo wengine, wanaimarishwa kuonyesha imani na upendo wa kutokeza. Wakati wa Utawala wa Milenia ya Kristo, watiwa-mafuta, wakiisha kufikia thawabu yao tukufu ya kimbingu, watatumiwa kama vyombo mkononi mwa Yehova ili kuinua uumbaji unaougua ufikie kiwango cha uhai wa milele.—Waroma 8:21, 22; Ufunuo 22:2.

      ‘Yehova Amekufurahia’

      9. Eleza jinsi hali ya Sayuni inavyogeuzwa.

      9 Upaji wa jina jipya ni sehemu ya kumgeuza Sayuni wa kimbingu, anayewakilishwa na watoto wake wa kidunia, ili awe na hali ya kupendeza. Tunasoma hivi: “Hutaitwa tena Aliyeachwa, wala nchi yako haitaitwa tena, Ukiwa; bali utaitwa Hefsiba [Namfurahia]; na nchi yako Beula [Ameolewa]; kwa kuwa BWANA anakufurahia, na nchi yako itaolewa.” (Isaya 62:4)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki