-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Isaya sura ya 52 hasa huwapa watu wa Mungu sababu ya kushangilia. Unabii wake unatimizwa juu ya Yerusalemu mwaka wa 537 K.W.K. Na una utimizo mkubwa zaidi unaohusisha “Yerusalemu la juu,” tengenezo la Yehova la kimbingu la viumbe-roho, ambalo nyakati nyingine hufafanuliwa kuwa mama na mke.—Wagalatia 4:26; Ufunuo 12:1.
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
2. Sayuni anaamka lini, na hilo linatukiaje?
2 Yehova anamtumia Isaya kupaza sauti akitoa mwito ufuatao kwa Sayuni, jiji Lake kipenzi: “Amka, amka, jivike nguvu zako, Ee Sayuni; jivike mavazi yako mazuri, Ee Yerusalemu, mji mtakatifu; kwa maana tokea sasa hataingia ndani yako asiyetahiriwa, wala aliye najisi. Jikung’ute mavumbi; uondoke, uketi, Ee Yerusalemu; jifungulie vifungo vya shingo yako, Ee binti Sayuni uliyefungwa.” (Isaya 52:1, 2)
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
3. Kwa nini kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta linaweza kuitwa “binti Sayuni,” nao wanakombolewa katika maana gani?
3 Maneno hayo ya Isaya yana utimizo unaohusu kutaniko la Kikristo pia. Kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta linaweza kufafanuliwa kuwa “binti Sayuni” wa kisasa, kwa kuwa “Yerusalemu la juu” ndiye mama yao.a Kwa kuwa watiwa-mafuta wamewekwa huru kutokana na mafundisho ya kipagani na ya uasi-imani, ni lazima wadumishe msimamo safi mbele za Yehova, si kwa kutahiriwa mwili, hapana, bali kwa kutahiriwa katika mioyo yao. (Yeremia 31:33; Waroma 2:25-29) Hiyo inahusisha kudumisha usafi wa kiroho, wa kiakili, na wa kiadili mbele za Yehova.—1 Wakorintho 7:19; Waefeso 2:3.
4. Ingawa “Yerusalemu la juu” halijakosa kamwe kumtii Yehova, ni mambo gani yaliyowapata wawakilishi wake duniani yanayofanana na yale ya wakaaji wa kale wa Yerusalemu?
4 Ni kweli kwamba “Yerusalemu la juu” halijakosa kamwe kumtii Yehova. Hata hivyo, wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, wawakilishi wake duniani—Wakristo watiwa-mafuta—walivunja sheria ya Yehova bila kujua kwa sababu hawakuuelewa vizuri msimamo wa kweli wa kutokuwamo kwa Kikristo. Walipoteza upendeleo wa kimungu, wakaingia katika utekwa wa kiroho wa “Babiloni Mkubwa,” ile milki ya ulimwengu ya dini ya uwongo. (Ufunuo 17:5) Upeo wa utumwa wao ulifika Juni 1918 wakati washirika wanane kati ya wafanyakazi wa Watch Tower Society walipofungwa gerezani kwa mashtaka ya uwongo, mojawapo likiwa ni kufanya uhaini. Hapo basi kazi ya kuhubiri habari njema kwa mpangilio mzuri ikawa ni kama imekoma. Lakini, mwaka wa 1919 mbiu ikapigwa kuwaita waamke kiroho. Wakristo watiwa-mafuta walianza kujitenga kwa ukamili zaidi na uchafu wa kiadili na wa kiroho wa Babiloni Mkubwa. Waliinuka kutoka kwenye mavumbi ya utekwa, nalo “Yerusalemu la juu” likapata fahari ya kuwa “mji mtakatifu” ambapo uchafu wa kiroho hauruhusiwi.
5. Kwa nini Yehova ana haki kamili ya kuwakomboa watu wake bila kuwapa watekaji wao malipo?
5 Mwaka wa 537 K.W.K. na pia mwaka wa 1919 W.K., Yehova alikuwa na haki kamili ya kuwakomboa watu wake. Isaya anaeleza hivi: “BWANA asema hivi, Mliuzwa bure; nanyi mtakombolewa bila fedha.” (Isaya 52:3) Babiloni wa kale wala Babiloni Mkubwa hakulipa chochote alipowatwaa watu wa agano la Mungu ili kuwamiliki wakiwa watumwa wao. Kwa kuwa mapatano ya kifedha hayakufanywa, bado Yehova ndiye aliyekuwa Mmiliki halali wa watu wake. Je, Yehova angalipaswa kuhisi kuwa ana deni la mtu yeyote? Hata kidogo. Katika visa vyote viwili, Yehova angeweza kuwa na haki ya kuwakomboa waabudu wake bila kuwapa watekaji wao malipo yoyote.—Isaya 45:13.
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
7. Utekwa wa watu wa Yehova umekuwa na matokeo gani juu ya jina lake?
7 Utekwa wa watu wa Yehova unaathiri jina lake, kama vile unabii unavyoonyesha: “Basi sasa, nafanya nini hapa [“ninapata faida gani hapa,” “NW”], asema BWANA, ikiwa watu wangu wamechukuliwa bure? Hao wanaowatawala wanapiga yowe, asema BWANA, na jina langu linatukanwa daima mchana kutwa. Kwa hiyo watu wangu watalijua jina langu kwa hiyo watajua siku ile ya kuwa mimi ndimi ninenaye; tazama ni mimi.” (Isaya 52:5, 6)
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
8. Jina la Yehova limetendewaje tangu mitume walipokufa?
8 Hayo yote yanahusuje “Yerusalemu la juu”? Tangu uasi-imani utie mizizi miongoni mwa wale wanaojiita Wakristo, ingeweza kusemwa kwamba “jina la Mungu linafanyiwa kufuru miongoni mwa mataifa kwa sababu ya [hao] watu.” (Waroma 2:24; Matendo 20:29, 30) Hivyo basi, hatimaye Wayahudi walianza kuepuka kutumia jina la Mungu kwa hofu ya kishirikina. Upesi baada ya kifo cha mitume, Wakristo waasi-imani walifuata mkondo huo huo wakaacha kulitumia jina la kibinafsi la Mungu. Jumuiya ya Wakristo, ambayo ni sehemu kubwa ya Babiloni Mkubwa, ilisitawi kutokana na uasi-imani huo. (2 Wathesalonike 2:3, 7; Ufunuo 17:5) Jina la Yehova limepata sifa mbaya kwa sababu ya ukosefu wa adili ulioenea sana katika Jumuiya ya Wakristo na hatia yake ya kumwaga damu kwa macho makavu.—2 Petro 2:1, 2.
9, 10. Watu wa agano la Mungu wa nyakati za kisasa wamepata uelewevu gani wa kina kirefu zaidi kuhusu viwango vya Yehova na jina lake?
9 Koreshi Mkubwa Zaidi, Yesu Kristo, alipowaweka huru watu wa agano la Mungu kutoka utekwa wa Babiloni Mkubwa mwaka wa 1919, waliyaelewa matakwa ya Yehova vizuri zaidi. Tayari walikuwa wamejisafisha kwa kuondoa mafundisho mengi ya Jumuiya ya Wakristo yaliyo na mizizi katika upagani wa nyakati zilizoutangulia Ukristo, kama vile Utatu, kutokufa kwa nafsi, na mateso ya milele katika helo yenye moto. Sasa walianza kujiondolea kabisa dalili zote za mavutano ya Kibabiloni. Pia wakaja kuutambua umuhimu wa kudumisha msimamo wa kutokuwamo kabisa katika mambo ya uzalendo wa ulimwengu huu. Hata walitaka kujitakasa kwa kuondoa hatia yoyote ya damu ambayo huenda ikawa baadhi yao walijiletea.
10 Pia watumishi wa kisasa wa Mungu walipata uelewevu wa kina kirefu zaidi juu ya umuhimu wa jina la Yehova. Mwaka wa 1931 walikubali kulitwaa jina Mashahidi wa Yehova, na hivyo wakatangaza peupe kwamba wanaunga mkono Yehova na jina lake. Zaidi ya hilo, kwa kuchapisha Biblia ya New World Translation tangu mwaka wa 1950, Mashahidi wa Yehova wamelirudisha jina la Mungu mahali pake katika Biblia. Naam, wao wamekuja kuthamini jina la Yehova na wanalijulisha mpaka miisho ya dunia.
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
11. Kwa nini inafaa kwamba sauti inapaazwa kusema “Mungu wako anamiliki!” kuhusiana na matukio ya mwaka wa 537 K.W.K.?
11 Sasa uangalifu wetu unageuzwa kumwelekea tena Sayuni akiwa bado katika ukiwa wake. Mjumbe anakaribia akiwa na habari njema: “Jinsi ilivyo mizuri [“yenye kupendeza,” “NW”] juu ya milima miguu yake aletaye habari njema, yeye aitangazaye amani, aletaye habari njema ya mambo mema, yeye autangazaye wokovu, auambiaye Sayuni, Mungu wako anamiliki!” (Isaya 52:7)
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Ingawa hivyo, leo mletaji huyo wa habari njema anajulikana. Yesu Kristo ndiye mjumbe mkubwa zaidi wa amani wa Yehova. Alipokuwa duniani, alizihubiri habari njema kwamba watu wangefunguliwa kabisa wasiwe na madhara ya dhambi iliyorithiwa kutoka kwa Adamu, baadhi yake yakiwa ni magonjwa na kifo. (Mathayo 9:35) Yesu aliweka mfano kwa kutia bidii kuzitangaza habari njema hizo za kitu kizuri zaidi, akatumia kila nafasi aliyopata kuwafundisha watu Ufalme wa Mungu. (Mathayo 5:1, 2; Marko 6:34; Luka 19:1-10; Yohana 4:5-26) Nao wanafunzi wake waliufuata mfano wake.
13. (a) Mtume Paulo anaelezaje kwa upana maana ya usemi ‘Jinsi ilivyo yenye kupendeza juu ya milima miguu yake aletaye habari njema’? (b) Kwa nini inaweza kusemwa kwamba miguu ya wajumbe hao ni “yenye kupendeza”?
13 Katika barua yake kwa Waroma, mtume Paulo ananukuu Isaya 52:7 kukazia umuhimu wa kazi ya kuzihubiri habari njema. Anatokeza mfululizo wa maswali yanayoamsha fikira, mojawapo likiwa ni ‘Watu watasikiaje bila mtu fulani kuhubiri?’ Halafu anasema hivi: “Kama vile imeandikwa: ‘Jinsi ilivyo yenye kupendeza miguu ya wale watangazao habari njema ya mambo mema!’” (Waroma 10:14, 15) Hivyo Paulo anapanua matumizi ya Isaya 52:7, akitumia neno “wale” kwa wingi, badala ya neno “yule” kwa umoja, linalopatikana katika maandishi-awali ya Isaya. Wakristo wote ni wajumbe wa habari njema za amani kwa kumwiga Yesu Kristo. Miguu yao ‘inapendeza’ jinsi gani? Isaya anaongea kana kwamba mpiga-mbiu anakaribia Yerusalemu kutoka kwenye milima ya Yuda iliyo karibu. Haiwezekani kuiona miguu ya mjumbe huyo kwa mbali. Hivyo basi, uangalifu hapa unaelekezwa kwenye mjumbe mwenyewe, kwani ile miguu inawakilisha mjumbe mwenyewe. Sawa na vile Yesu na wanafunzi wake walivyokuwa na sura maridadi kwa watu wasikivu karne ya kwanza, Mashahidi wa kisasa ni wenye kupendeza machoni pa watu wanyenyekevu wanaousikiza ujumbe wa habari njema unaookoa uhai.
14. Yehova amekuwaje Mfalme nyakati za kisasa, na ni tangu lini wanadamu wametangaziwa jambo hilo?
14 Ni tangu lini katika nyakati za kisasa sauti imesikika ikipaazwa kusema “Mungu wako anamiliki!”? Ni tangu mwaka wa 1919. Mwaka huo, kwenye mkusanyiko fulani Cedar Point, Ohio, J. F. Rutherford, msimamizi wa Watch Tower Society wakati huo, aliwachochea wasikilizaji wake kwa hotuba yenye kichwa “Hotuba kwa Wafanyakazi Wenzi.” Hotuba hiyo, ambayo msingi wake ulikuwa Isaya 52:7 na Ufunuo 15:2, iliwatia moyo wahudhuriaji wote waanze kazi ya kuhubiri. Hivyo, ‘miguu yenye kupendeza’ ilianza kuonekana ‘milimani.’ Kwanza Wakristo watiwa-mafuta, na baadaye waandamani wao wa “kondoo wengine,” walijitokeza kwenda kuzihubiri habari njema kwamba Yehova amekuwa Mfalme. (Yohana 10:16) Yehova akawa Mfalme jinsi gani? Alionyesha kwamba amekuwa mfalme kwa njia mpya mwaka wa 1914 alipomtawaza Mwanawe, Yesu Kristo, awe Mfalme katika Ufalme wa kimbingu uliokuwa umeanzishwa karibuni. Kisha Yehova akafanya wonyesho mwingine wa utawala wake wa kifalme mwaka wa 1919 alipokomboa “Israeli wa Mungu” kutoka Babiloni Mkubwa.—Wagalatia 6:16; Zaburi 47:8; Ufunuo 11:15, 17; 19:6.
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
15. “Walinzi” wanaopaza sauti yao mwaka wa 537 K.W.K. ni akina nani?
15 Je, kule kupaza sauti kwamba “Mungu wako anamiliki!” kunatokeza itikio fulani? Ndiyo. Isaya anaandika hivi: “Sauti ya walinzi wako! Wanapaza sauti zao, wanaimba pamoja; maana wataona jicho kwa jicho, jinsi BWANA arejeavyo Sayuni.” (Isaya 52:8)
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
17, 18. (a) Jamii ya kisasa ya mlinzi imepazaje sauti yake? (b) Ni katika maana gani jamii ya mlinzi imetoa mwito kwa kupaaza sauti pamoja?
17 Katika utimizo wa kisasa, jamii ya mlinzi, yaani yule “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” inapaza sauti yake, si kuwaelekea wale tu ambao tayari wamo katika tengenezo la Mungu linaloonekana, bali pia kuwaelekea watu wa nje. (Mathayo 24:45-47) Mwaka wa 1919 mwito ulitokezwa kuwakusanya watiwa-mafuta waliobakia, kisha mwito huo ukakaziwa mwaka wa 1922 kwenye mkusanyiko wa Cedar Point, Ohio, kwa ombi lililosema “tangazeni, tangazeni, tangazeni, Mfalme na ufalme wake.” Tangu mwaka wa 1935, fikira zimeelekezwa hasa kwenye kazi ya kukusanya umati mkubwa wa watu walio kama kondoo. (Ufunuo 7:9, 10) Miaka ya hivi majuzi tangazo linalohusu utawala wa ufalme wa Yehova limetiliwa nguvu zaidi. Jinsi gani? Mwaka wa 2000, watu wapatao milioni sita walikuwa wakishiriki kutangaza utawala wa Ufalme wa Yehova katika nchi na maeneo zaidi ya 230. Isitoshe, Mnara wa Mlinzi, chombo kikuu kinachotumiwa na jamii ya mlinzi, kinapaaza sauti ya ujumbe huo wenye shangwe katika lugha zaidi ya 130.
18 Unyenyekevu na upendo wa kidugu unahitajiwa ili kushiriki katika kazi hiyo ya kuleta umoja. Ili mwito uwe na matokeo mazuri, ni lazima wahusika wote wauhubiri ujumbe ule ule mmoja, wakikazia jina la Yehova, uandalizi wake wa fidia, hekima yake, upendo wake, na Ufalme wake. Wakristo wote ulimwenguni kote wanapofanya kazi bega kwa bega, kifungo cha uhusiano wao binafsi na Yehova kinaimarishwa ili kuvumisha pamoja habari za mteremo.
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
19. (a) “Mahali pa Yerusalemu palipokuwa ukiwa” panakuwaje na kelele za furaha? (b) Yehova ‘ameuweka wazi mkono wake mtakatifu’ katika maana gani?
19 Huku watu wa Mungu wakiwa wanapaaza sauti kwa shangwe, hata makao yao yenyewe yanaonekana yakipiga kelele kwa furaha. Unabii unaendelea kusema hivi: “Pigeni kelele za furaha, imbeni pamoja [“kwa shangwe,” “NW”], enyi mahali pa Yerusalemu palipokuwa ukiwa; kwa kuwa BWANA amewafariji watu wake, ameukomboa Yerusalemu. BWANA ameweka wazi mkono wake mtakatifu machoni pa mataifa yote; na ncha zote za dunia zitauona wokovu wa Mungu wetu.” (Isaya 52:9, 10)
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
20. Kumekuwako na bado kutakuwako matokeo gani kwa sababu Yehova ameuweka mkono wake ukiwa wazi nyakati za kisasa?
20 Katika hizi “siku za mwisho,” Yehova ameuweka wazi mkono wake mtakatifu ili kuwahuisha mabaki watiwa-mafuta, wale ‘mashahidi wawili’ wa kitabu cha Ufunuo. (2 Timotheo 3:1; Ufunuo 11:3, 7-13) Tangu mwaka wa 1919, wameingizwa katika paradiso ya kiroho, makao ya kiroho wanayoyashiriki sasa pamoja na mamilioni ya washirika wao, wale kondoo wengine. Mwishowe, Yehova atauweka wazi mkono wake mtakatifu awaletee watu wake wokovu kwenye “Har-Magedoni.” (Ufunuo 16:14, 16) Hapo ndipo “ncha zote za dunia zitauona wokovu wa Mungu wetu.”
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
21. (a) Wale ‘wanaochukua vyombo vya Yehova’ wanatakiwa wafanye nini? (b) Kwa nini Wayahudi wanaoondoka Babiloni hawana sababu ya kubabaika kwa hofu?
21 Wale wanaotoka Babiloni kurudi Yerusalemu wana takwa fulani la kutimiza. Isaya anaandika hivi: “Nendeni zenu, nendeni zenu, tokeni huko, msiguse kitu kichafu; tokeni kati yake; iweni safi ninyi mnaochukua vyombo vya BWANA. Maana hamtatoka kwa haraka [“kubabaika kwa hofu,” “NW”], wala hamtakwenda kwa kukimbia, kwa sababu BWANA atawatangulia; na Mungu wa Israeli atawafuata nyuma; awalinde.” (Isaya 52:11, 12)
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
22. Paulo anakaziaje uhitaji wa usafi miongoni mwa Wakristo watiwa-mafuta?
22 Maneno ya Isaya kuhusu kuendelea kuwa safi yanatimizwa kwa kadiri kubwa juu ya wazao wa “Yerusalemu la juu.” Paulo alipowaonya kwa upole Wakristo Wakorintho wasifungwe nira pamoja na wasio waamini kwa njia isiyosawazika, aliyanukuu maneno ya Isaya 52:11: “‘Kwa hiyo tokeni miongoni mwao, na jitengeni wenyewe,’ asema Yehova, ‘na komeni kugusa kitu kisicho safi.’” (2 Wakorintho 6:14-17) Sawa na vile ilivyokuwa kwa Waisraeli wakielekea nyumbani kutoka Babiloni, ni lazima Wakristo waepuke kabisa ibada ya uwongo ya Kibabiloni.
23. Watumishi wa Yehova leo hujitahidi kujidumisha wakiwa safi kwa njia zipi?
23 Ndivyo hasa ilivyokuwa kwa habari ya wale wafuasi watiwa-mafuta wa Yesu Kristo waliokimbia kutoka Babiloni Mkubwa mwaka wa 1919. Walijisafisha hatua kwa hatua wakajiondolea dalili zote zilizobaki za ibada ya uwongo. (Isaya 8:19, 20; Waroma 15:4) Pia walipata ufahamu zaidi kuhusu umuhimu wa usafi wa kiadili. Ingawa nyakati zote Mashahidi wa Yehova wametetea viwango vya juu vya kiadili, mwaka wa 1952 gazeti Mnara wa Mlinzi lilikuwa na makala zilizokazia uhitaji wa kuwatia nidhamu wakosefu wa adili ili kudumisha usafi wa kutaniko. Hatua hiyo ya nidhamu humsaidia mkosaji mwenyewe atambue uhitaji wa kutubu kwa moyo mweupe.—1 Wakorintho 5:6, 7, 9-13; 2 Wakorintho 7:8-10; 2 Yohana 10, 11.
24. (a) ‘Vyombo vya Yehova’ ni nini nyakati za kisasa? (b) Kwa nini Wakristo leo wana uhakika kwamba Yehova ataendelea kutangulia mbele yao na pia awe mlinzi nyuma yao?
24 Wakristo watiwa-mafuta pamoja na ule umati mkubwa wa kondoo wengine wamepiga moyo konde kutogusa kitu chochote chenye uchafu wa kiroho. Hali yao iliyotiwa utakato na usafi huwastahilisha wawe wachukuaji wa ‘vyombo vya Yehova.’ Vyombo hivyo ni yale maandalizi ya thamani kubwa ambayo Mungu hufanya ili yatumiwe katika utumishi mtakatifu wa huduma ya nyumba kwa nyumba na ya funzo la Biblia na namna nyingine za utendaji wa Kikristo. Kwa kudumisha msimamo safi, watu wa Mungu leo wanaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova ataendelea kutangulia mbele yao na vilevile awe mlinzi nyuma yao. Kwa kuwa wao ni watu safi wa Mungu, wana sababu tele za ‘kuimba pamoja kwa shangwe’!
-