Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • “Tazama, Watumishi Wangu Watafurahi”

      16. Yehova atawabariki watumishi wake waaminifu kwa njia zipi, lakini itakuwaje kwa wale ambao wamemwacha?

      16 Unabii unaeleza kwamba kuna thawabu tofauti-tofauti ambazo zinawangoja wale wanaomwabudu Mungu kwa moyo mweupe na wale wanaofanya hivyo kwa unafiki. Unafanya hivyo kwa kuwakaripia wale ambao wamemwacha Yehova: “Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, watumishi wangu watakula, bali ninyi mtaona njaa; tazama, watumishi wangu watakunywa, bali ninyi mtaona kiu; tazama, watumishi wangu watafurahi, bali ninyi mtatahayarika; tazama, watumishi wangu wataimba kwa furaha [“hali njema,” “NW”] ya moyo, bali ninyi mtalia kwa huzuni ya moyo; mtapiga kelele kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.” (Isaya 65:13, 14) Yehova atawabariki watumishi wake waaminifu. Wakiwa na mioyo inayofurika shangwe, watabubujika kelele za furaha. Kula, kunywa, na kufurahi ni maneno yanayoonyesha kwamba Yehova atatosheleza mahitaji ya waabudu wake kwa vitu kemkemu. Tofauti na hivyo, wale ambao wamechagua kumwacha Yehova wataona njaa na kiu ya kiroho. Mahitaji yao hayatatoshelezwa. Watalia kwa sauti kubwa na kupiga makelele ya kuomboleza kwa uchungu na msononeko.

      17. Kwa nini watu wa Mungu leo wana sababu nzuri ya kuimba kwa furaha?

      17 Maneno ya Yehova yanaieleza vizuri hali ya kiroho ya watu ambao leo wanadai kwa maneno tu kwamba wanamtumikia Mungu. Hata ingawa mamilioni ya watu wa Jumuiya ya Wakristo wana uchungu wa roho, waabudu wa Yehova wanaimba kwa furaha. Nao wana sababu nzuri ya kushangilia. Wanalishwa vema kiroho. Yehova huwaandalia chakula kingi cha kiroho kupitia vichapo vya Kibiblia na makusanyiko ya Kikristo. Kwa hakika, zile kweli zenye kujenga na ahadi zenye faraja zilizo katika Neno la Mungu hutupatia ‘hali njema ya moyo’!

  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 21. Ni mbingu mpya zipi zilizotokea mwaka wa 1914?

      21 Hata hivyo, kumbuka kwamba Petro alirudia maneno ya unabii wa Isaya akaonyesha kwamba ungetimizwa wakati ujao. Mtume huyo aliandika hivi: “Ziko mbingu mpya na dunia mpya ambazo tunangojea kulingana na ahadi yake, na katika hizo uadilifu utakaa.” (2 Petro 3:13) Mwaka wa 1914 zile mbingu mpya zilizokuwa zimengojewa sana zilitokea. Ufalme wa Kimesiya uliozaliwa mwaka huo unatawala kutoka mbinguni kwenyewe, na Yehova ameupa ufalme huo mamlaka ya kuitawala dunia yote. (Zaburi 2:6-8) Serikali hiyo ya Ufalme, iliyo chini ya Kristo na watawala wenzake 144,000, ndio mbingu mpya.—Ufunuo 14:1.

      22. Dunia mpya itafanyizwa kwa watu gani, na watu wanatayarishwaje hata sasa ili wawe kiini cha mpango huo?

      22 Namna gani dunia mpya? Kwa kufuata kielelezo cha utimizo wa kale, dunia mpya itafanyizwa kwa watu wanaofurahia kujitiisha chini ya utawala wa serikali mpya ya kimbingu. Hata sasa, mamilioni ya watu mmoja-mmoja wenye mwelekeo unaofaa wananyenyekea chini ya serikali hiyo na kujitahidi kufuata sheria zake zilizo katika Biblia. Wanatoka katika taifa zote, lugha zote, na jamii zote, nao hushirikiana kumtumikia Mfalme Yesu Kristo anayetawala. (Mika 4:1-4) Mfumo mwovu wa mambo uliopo ukiisha kupita, kikundi hicho ndicho kitakachofanyizwa kuwa kiini cha dunia mpya na hatimaye kiwe jamii ya wanadamu wenye kumhofu Mungu watakaokuwa kila mahali ulimwenguni, wakiwa warithi wa makao ya kidunia ya Ufalme wa Mungu.—Mathayo 25:34.

  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Kupitia Isaya, Yehova anasema hivi: “Tazama, mimi ninaumba mbingu mpya na dunia mpya, na maneno ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni.” (Isaya 65:17, “Zaire Swahili Bible”)

  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • “Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake. Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.” (Isaya 65:21, 22)

  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 24. Kwa nini Yehova atashangilia kurudishwa kwa Yerusalemu, na ni nini ambacho hakitasikiwa tena katika barabara za jiji?

      24 Unabii wa Isaya unaendelea kusema hivi: “Furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha. Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza.” (Isaya 65:18, 19)

  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 25, 26. (a) Katika siku zetu, Yehova anafanyaje Yerusalemu liwe “shangwe”? (b) Yehova atatumia Yerusalemu Jipya kwa njia gani, na kwa nini sisi tunaweza kushangilia leo?

      25 Leo, pia, Yehova anafanya Yerusalemu liwe “shangwe.” Jinsi gani? Kama vile tumekwisha kuona, hatimaye zile mbingu mpya zilizotokea mwaka wa 1914 zitahusisha pia watawala wenzi 144,000, wenye kushiriki katika ile serikali ya kimbingu. Mbingu hizo zinatajwa kiunabii kuwa “Yerusalemu Jipya.” (Ufunuo 21:2) Yerusalemu Jipya ndilo linalomaanishwa wakati Mungu anaposema hivi: “Tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha.” Yerusalemu Jipya litatumiwa na Mungu kuwamiminia wanadamu watiifu baraka zisizo na kifani. Haitasikiwa tena sauti ya kulia wala ya maombolezo, kwa maana Yehova atatosheleza “haja za moyo [wetu].”—Zaburi 37:3, 4.

      26 Kwa kweli, sisi leo tuna sababu kamili ya kufurahi sana! Karibuni Yehova atatakasa jina lake maarufu kwa kuwaharibu wapinzani wote. (Zaburi 83:17, 18) Kisha mbingu mpya peke yake zishike usukani kusimamia mambo yote. Lo, hizo ni sababu nzuri kama nini za kufurahi sana na kukishangilia milele kile kinachoumbwa na Mungu!

  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 30. Watumishi wa Yehova wanafurahia hali gani leo, na watafurahia nini katika ulimwengu mpya?

      30 Unabii huu umepata utimizo fulani katika siku zetu. Watu wa Yehova walitoka kwenye uhamisho wa kiroho mwaka wa 1919, wakaanza kurudisha hali za kwanza katika “nchi” au makao yao ya utendaji na ibada. Walijenga makutaniko na kusitawisha hali ya kuzaa matunda ya kiroho. Matokeo ni kwamba, hata sasa watu wa Yehova wanafurahia paradiso ya kiroho na amani waliyopewa na Mungu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki