-
Kutafuta Hali ya KirohoMnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
-
-
Kamusi moja inafafanua hali ya kiroho kuwa “kutambua uhitaji wa au kushikamana na viwango vya kidini” na pia “sifa au hali ya kuwa mtu wa kiroho.” Hivyo, maneno kama vile “hali ya kiroho,” “kuwa mtu wa kiroho,” na “kuwa makini kiroho” yanaonwa kuwa yanamaanisha jambo lilelile. Ili kufafanua zaidi maneno “hali ya kiroho,” fikiria ulinganisho huu: Mtu aliye stadi katika biashara anasemwa kuwa makini kibiashara. Vivyo hivyo, mtu anayethamini sana mambo ya kiroho au ya kidini anasemwa kuwa makini kiroho.
-
-
Kutafuta Hali ya KirohoMnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
-
-
Wanadai kwamba kuwa mtu wa kiroho kunamaanisha, “kuamini bila kuwa mshiriki,” yaani, kuamini kwamba kuna mungu bila kujiunga na kanisa lolote. Wengine wanaona kwamba kuwa mtu wa kiroho, si kuwa mwanadini, bali ni kutamani kuwa na amani ya ndani na kusudi maishani. Wanadai kwamba wale wanaojitahidi kuwa watu wa kiroho hawahitaji dini hata kidogo. Badala ya kumwendea Mungu au dini wanahitaji tu kufuata hisia zao za ndani ili kuwa watu wa kiroho. Mwandikaji mmoja anasema hivi: “Hali ya kiroho ya kweli ni hali inayopatikana ndani sana ya mtu. Ni jinsi unavyopenda, unavyokubali, na unavyochangamana na ulimwengu na watu walio karibu nawe. Haiwezi kupatikana kanisani au kwa kufuata imani fulani.”
-
-
Hali ya Kiroho ya Kweli Unaweza Kuipata Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
-
-
Zaidi ya kuonyesha umuhimu na faida za kukaza akili juu ya mambo ya kiroho, mtume Paulo alisema mengi kuhusu maana ya hali ya kiroho ya kweli. Paulo aliwaeleza Wakristo katika jiji la kale la Korintho tofauti iliyopo kati ya mtu wa kimwili, yaani, mtu anayefuata tamaa za mwili, na mtu wa kiroho, yule anayethamini mambo ya kiroho. Paulo aliandika: “Mtu wa kimwili hayapokei mambo ya roho ya Mungu, kwa maana hayo ni upumbavu kwake.” Kwa upande mwingine, Paulo alieleza kwamba mtu wa kiroho ana “akili ya Kristo.”—1 Wakorintho 2:14-16.
Kuwa na “akili ya Kristo” kunamaanisha hasa kuwa na ‘mtazamo wa akili ambao ulikuwa pia ndani ya Kristo Yesu.’ (Waroma 15:5; Wafilipi 2:5) Kwa maneno mengine, mtu wa kiroho ni yule anayefikiri kama Yesu na anayetembea katika hatua Zake. (1 Petro 2:21; 4:1)
-
-
Hali ya Kiroho ya Kweli Unaweza Kuipata Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
-
-
Hali ya Kiroho na “Matunda ya Roho”
Luka, mwandikaji wa Injili, alisema kwamba Yesu alipobatizwa, alimiminiwa roho ya Mungu na kwamba Yesu alikuwa “amejaa roho takatifu.” (Luka 3:21, 22; 4:1) Naye Yesu alikazia akilini mwa wafuasi wake umuhimu wa kuongozwa na roho takatifu ya Mungu, au ‘nguvu zake za utendaji.’ (Mwanzo 1:2; Luka 11:9-13) Kwa nini hilo ni jambo la maana? Ni kwa sababu roho ya Mungu ina nguvu ya kubadili akili ya mtu, ili ianze kufanana na akili ya Kristo. (Waroma 12:1, 2) Roho takatifu inatokeza ndani ya mtu sifa kama vile “upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujizuia.” Sifa hizo, ambazo Biblia inaziita “matunda ya roho,” zinaonyesha kwamba mtu fulani ni mtu wa kiroho kikweli. (Wagalatia 5:22, 23) Kwa ufupi, mtu aliye makini kiroho ni yule anayeongozwa na roho ya Mungu.
-
-
Hali ya Kiroho ya Kweli Unaweza Kuipata Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
-
-
Hali ya Kiroho na Sala
Masimulizi ya Injili yanaonyesha kwamba Yesu alisali kwa Mungu kwa ukawaida. (Marko 1:35; Luka 5:16; 22:41) Katika huduma yake hapa duniani, Yesu alitenga wakati wa kusali. Mwanafunzi Mathayo aliandika: “Baada ya kuwaruhusu umati waende zao, [Yesu] akapanda mlimani akiwa peke yake ili kusali.” (Mathayo 14:23) Yesu alipata nguvu kutokana na pindi hizo tulivu ambazo alitumia kuzungumza na Baba yake wa mbinguni. (Mathayo 26:36-44) Vivyo hivyo leo, watu walio makini kiroho wanatafuta nafasi za kuzungumza na Mungu, wakijua kwamba hilo litaimarisha uhusiano wao na Muumba na kuwawezesha kuwa na akili kama ya Kristo.
Mara nyingi Yesu alisali kwa muda mrefu. (Yohana 17:1-26) Kwa mfano, kabla ya kuwachagua wanaume 12 waliokuja kuwa mitume wake, Yesu “alienda mlimani kusali, naye akaendelea kusali kwa Mungu usiku wote.” (Luka 6:12) Ingawa si lazima wasali usiku wote, wale walio makini kiroho wanafuata mfano wa Yesu. Kabla ya kufanya maamuzi makubwa maishani, wanatumia muda wa kutosha kusali kwa Mungu, wakiomba roho takatifu iwaongoze kufanya maamuzi yatakayoboresha hali yao ya kiroho.
Kupitia sala zake, Yesu alionyesha bidii ambayo tunapaswa kuwa nayo tunaposali. Ona yale ambayo Luka aliandika kuhusu jinsi Yesu alivyosali jioni iliyotangulia kifo chake. “Akaingia katika maumivu makali, akaendelea kusali kwa bidii zaidi; na jasho lake likawa kama matone ya damu yakianguka chini.” (Luka 22:44) Yesu aliwahi kusali kwa bidii, lakini pindi hii, akikabili jaribu kali zaidi katika maisha yake hapa duniani, alisali “kwa bidii zaidi” na sala yake ikajibiwa. (Waebrania 5:7) Watu walio makini kiroho wanafuata mfano wa Yesu. Wanapokabili majaribu makali zaidi, wanasali “kwa bidii zaidi” kwa Mungu ili awape roho takatifu, mwongozo, na utegemezo.
Kwa kuwa ni wazi kwamba Yesu alisali mara nyingi, haishangazi kwamba wanafunzi wake walitaka kumwiga. Hivyo, walimwomba hivi: “Bwana, tufundishe jinsi ya kusali.” (Luka 11:1) Vivyo hivyo leo, wale wanaothamini mambo ya kiroho na wanataka kuongozwa na roho takatifu ya Mungu wanafuata mfano wa Yesu wanaposali kwa Mungu. Hali ya kiroho ya kweli inahusiana sana na sala.
-
-
Hali ya Kiroho ya Kweli Unaweza Kuipata Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
-
-
Leo, bado kazi ya kuwaambia wengine kuhusu Ufalme wa Mungu inawatambulisha wale walio na akili ya Kristo. Yesu aliwapa amri hii watu wote wanaotaka kuwa wafuasi wake: “Nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, . . . na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.” (Mathayo 28:19, 20) Kwa kuongezea, Yesu alitabiri hivi: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14) Kwa kuwa Neno la Mungu linaonyesha kwamba kazi ya kuhubiri inafanywa kwa nguvu za roho takatifu, kushiriki kwa bidii katika kazi hiyo kunaonyesha kwamba mtu ana hali ya kiroho ya kweli.—Matendo 1:8.
-
-
Hali ya Kiroho ya Kweli Unaweza Kuipata Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
-
-
[Picha/Sanduku katika ukurasa wa 7]
ALAMA ZA HALI YA KIROHO
◆ Kupenda Neno la Mungu
◆ Kuonyesha matunda ya roho
◆ Kusali kwa Mungu kwa ukawaida na kwa bidii
◆ Kuwahubiria wengine habari njema ya Ufalme
-