Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Walio Wazee Ni Washiriki Wenye Thamani wa Undugu Wetu wa Kikristo
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Mei 15
    • [Sanduku katika ukurasa wa 13]

      Jinsi Ambavyo Wamedumisha Afya Katika Imani

      Ni nini ambacho kimewasaidia Wakristo wa muda mrefu waendelee kuwa na afya katika imani na kudumisha nguvu za kiroho? Baadhi yao wamesema hivi:

      “Ni muhimu sana kusoma maandiko yanayokazia uhusiano wetu pamoja na Yehova. Mara nyingi usiku, mimi hukariri Zaburi ya 23 na 91.”—Olive, aliyebatizwa mwaka wa 1930.

      “Nimehakikisha kwamba ninahudhuria kila hotuba ya ubatizo na kusikiliza kwa makini, kana kwamba mimi ndiye ninayebatizwa. Kuendelea kufikiria ubatizo wangu kumenisaidia kubaki mwaminifu.”—Harry, aliyebatizwa mwaka wa 1946.

      “Ni muhimu kusali kila siku—sikuzote tukiomba msaada, ulinzi, na baraka za Yehova, ‘tukimtambua katika njia zetu zote.’” (Methali 3:5, 6)—Antônio, aliyebatizwa mwaka wa 1951.

      “Kusikiliza mambo yaliyoonwa kutoka kwa wale ambao bado wanamtumikia Yehova kwa uaminifu baada ya miaka mingi, hufanya niazimie kudumisha uaminifu na ushikamanifu wangu kwake.”—Joan, aliyebatizwa mwaka wa 1954.

      “Si vizuri kujifikiria kupita kiasi. Kila kitu tulicho nacho kinatokana na fadhili zisizostahiliwa za Mungu. Kuwa na maoni hayo hutusaidia tutafute chakula cha kiroho mahali panapofaa ili kuvumilia hadi mwisho.”—Arlene, aliyebatizwa mwaka wa 1954.

  • Walio Wazee Ni Washiriki Wenye Thamani wa Undugu Wetu wa Kikristo
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Mei 15
    • “Wataendelea Kuwa Wanono na Wabichi”

      9, 10. Wakristo walio wazee huendeleaje kuwa wenye afya katika imani na kudumisha nguvu za kiroho? (Ona sanduku kwenye ukurasa wa 13.)

      9 Akikazia jinsi watumishi wa Yehova walio wazee wanavyozaa matunda, mtunga-zaburi aliimba: “Mwadilifu atachanua kama mtende; kama mwerezi katika Lebanoni, atakuwa mkubwa. Bado wataendelea kusitawi wakati wa kuwa na kichwa chenye mvi, wataendelea kuwa wanono na wabichi.”—Zaburi 92:12, 14.

      10 Unawezaje kudumisha nguvu zako za kiroho licha ya kuzeeka? Mtende utadumisha umaridadi wake tu iwapo utapata maji ya kutosha. Vivyo hivyo, unaweza kutegemezwa na maji ya kweli za Biblia kwa kujifunza Neno la Mungu na kwa kushirikiana na tengenezo lake. (Zaburi 1:1-3; Yeremia 17:7, 8) Unakuwa mwenye thamani kwa waabudu wenzako unapokuwa na nguvu za kiroho. Fikiria jinsi jambo hilo linavyothibitishwa na kielelezo cha Kuhani Mkuu Yehoyada aliyekuwa mzee.

      11, 12. (a) Yehoyada alitimiza fungu gani muhimu katika historia ya ufalme wa Yuda? (b) Yehoyada alitumiaje mamlaka yake kuendeleza ibada ya kweli?

      11 Labda Yehoyada alikuwa na umri wa miaka zaidi ya mia moja wakati Malkia Athalia mwenye kutaka makuu alipoanza kutawala Yuda baada ya kuwaua wajukuu wake. Mzee Yehoyada angefanya nini? Kwa miaka sita, yeye na mke wake walimficha hekaluni Yehoashi, mrithi pekee wa kiti cha ufalme aliyeokoka. Kisha, katika hatua ya kushangaza, Yehoyada akamtangaza Yehoashi mwenye umri wa miaka saba kuwa mfalme na kuagiza Athalia auawe.—2 Mambo ya Nyakati 22:10-12; 23:1-3, 15, 21.

      12 Akiwa mlinzi wa mfalme, Yehoyada alitumia mamlaka yake kuendeleza ibada ya kweli. ‘Alifanya agano kati yake na watu wote na mfalme kwamba wao wataendelea kuwa watu wa Yehova.’ Yehoyada aliwaagiza watu wabomoe nyumba ya mungu wa uwongo Baali, waondoe madhabahu yake, sanamu, na kuhani wake. Pia Yehoashi alirudisha huduma za hekalu na kulifanyia ukarabati uliohitajiwa sana chini ya mwongozo wa Yehoyada. ‘Yehoashi aliendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova siku zake zote ambazo Yehoyada kuhani alimfundisha.’ (2 Mambo ya Nyakati 23:11, 16-19; 24:11-14; 2 Wafalme 12:2) Yehoyada alipokufa akiwa na umri wa miaka 130, alipewa heshima ya kipekee kwa kuzikwa pamoja na wafalme kwa sababu “alikuwa ametenda mema katika Israeli na kwa Mungu wa kweli na kwa nyumba Yake.”—2 Mambo ya Nyakati 24:15, 16.

      13. Wakristo walio wazee wanawezaje ‘kutenda mema kwa Mungu wa kweli na kwa nyumba yake’?

      13 Labda afya mbaya au hali nyingine zinapunguza yale unayoweza kufanya ili kuendeleza ibada ya kweli. Hata kama hali yako iko hivyo, bado unaweza ‘kutenda mema kwa Mungu wa kweli na kwa nyumba yake.’ Unaweza kuwa mwenye bidii kwa ajili ya nyumba ya Yehova kwa kuhudhuria na kutoa maelezo katika mikutano ya kutaniko na kwa kushiriki katika huduma ya shambani inapowezekana. Kuwa tayari kukubali shauri la Biblia na kumuunga mkono kwa ushikamanifu “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” na kutaniko pia, kutawaimarisha ndugu zako Wakristo. (Mathayo 24:45-47) Pia unaweza kuwachochea waabudu wenzako “katika upendo na matendo mazuri.” (Waebrania 10:24, 25; Filemoni 8, 9) Nawe utawanufaisha wengine ukifuata shauri hili la mtume Paulo: “Wanaume wenye umri mkubwa wawe na kiasi katika mazoea, wenye kuchukua mambo kwa uzito, wenye utimamu wa akili, wenye afya katika imani, katika upendo, katika uvumilivu. Vivyo hivyo wanawake wenye umri mkubwa wawe wenye tabia ya kumhofu Mungu, si wachongezi, wala si watumwa wa divai nyingi sana, wawe walimu wa yaliyo mema.”—Tito 2:2-4.

      14. Waangalizi Wakristo ambao wametumikia kwa muda mrefu wanaweza kufanya nini ili kuendeleza ibada ya kweli?

      14 Je, umetumikia ukiwa mzee wa kutaniko kwa miaka mingi? “Tumia hekima ambayo umejipatia kwa miaka mingi bila ubinafsi,” ndivyo anavyoshauri mzee mmoja wa kutaniko ambaye ametumikia kwa muda mrefu. “Wakabidhi wengine madaraka, na kushiriki ujuzi wako pamoja na wale walio tayari kujifunza . . . Tambua uwezo wa wengine. Uongeze na kuukuza uwezo huo. Jitayarishe kwa ajili ya wakati ujao.” (Kumbukumbu la Torati 3:27, 28) Ikiwa unapendezwa kikweli na kazi ya kuhubiri Ufalme inayozidi kupanuka, utawanufaisha sana wengine katika undugu wetu wa Kikristo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki