-
Dyslexia Haijanizuia Kufikia Miradi YanguAmkeni!—2009 | Februari
-
-
Ili nijifunze haraka zaidi, niliamua kuhamia Sri Lanka, nchi ambayo Kitamili kinazungumzwa na mamilioni ya watu.
Nilipofika Sri Lanka mnamo Oktoba (Mwezi wa 10) 1996, kulikuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Kwa muda fulani, niliishi katika mji wa Vavuniya uliokuwa kati ya vikundi viwili vilivyokuwa vikipigana. Mashahidi wa eneo hilo hawakuwa na vitu vingi vya kimwili, lakini walikuwa na upendo na ukarimu mwingi sana, nao walijaribu sana kunifundisha Kitamili. Watu ambao si Mashahidi walivutiwa sana kwamba mzungu pekee katika eneo lao alikuwa akijaribu kuzungumza lugha yao. Kwa kuwa walithamini sana mambo na walikuwa wanyenyekevu, ilikuwa rahisi zaidi kwangu kuzungumza nao kuhusu Biblia.
Mnamo Januari 1997, nilihitaji kurudi Denmark, na mwaka uliofuata, nilimwoa Camilla, ambaye alikuwa painia. Nilitamani sana kurudi Sri Lanka, hivyo, Desemba 1999, nilirudi nikiwa pamoja na mke wangu. Muda si muda, tulikuwa tukijifunza Biblia na familia na watu kadhaa, na tuliandamana na Mashahidi wa eneo hilo kwenye mafunzo yao ya Biblia. Tulikuwa tumezama kabisa katika huduma na lugha ya huko.
Machi (Mwezi wa 3) 2000, ilibidi turudi Denmark. Ilikuwa vigumu sana kuwaacha Mashahidi wenzetu na wanafunzi wa Biblia kwani tuliwapenda sana.
-
-
Dyslexia Haijanizuia Kufikia Miradi YanguAmkeni!—2009 | Februari
-
-
[Picha katika ukurasa wa 23]
Nikiwa na Shahidi mwenzangu huko Sri Lanka
-