-
Michezo ya Olimpiki Yarudi NyumbaniAmkeni!—2004 | Agosti 8
-
-
Mshindi wa Dhahabu Ni . . .
Fataki zitakapolipuliwa kwenye sherehe za ufunguzi za mashindano hayo, macho yote yataelekezwa kwenye Uwanja wa Olimpiki unaotoshea watu 75,000. Kwa wengi, uwanja huo uliorekebishwa ndio sehemu ya pekee zaidi kati ya vituo vyote vya Olimpiki huko Athens. Kinachofanya uwanja huo kuwa wa pekee ni paa yake iliyobuniwa na Santiago Calatrava, msanifu-ujenzi maarufu kutoka Hispania.
Paa hiyo ni kazi bora ya sanaa kwani imetengenezwa kwa vioo vyenye uzito wa tani 16,000 na ina ukubwa wa meta 10,000 za mraba. Itashikiliwa na matao mawili makubwa sana kila moja likiwa na urefu wa meta 304 na kimo cha meta 80—imezidi ukubwa wa Daraja la Bandari ya Sydney huko Australia kwa thuluthi mbili! Kulingana na mtaalamu mmoja wa ujenzi, kila chuma kilichotumiwa kutengeneza matao hayo kina uzito wa kati ya tani 9,000 na 10,000 na “kina upana mkubwa kuliko basi.” Inatazamiwa kwamba uzito wa paa hiyo utakuwa mara mbili ya ule wa Mnara wa Eiffel huko Paris.
Kwa nini paa kubwa sana hivyo inahitajiwa? Fikiria joto kali la mwezi wa Agosti huko Athens! Vioo hivyo vimetandazwa rangi ya pekee inayorudisha asilimia 60 ya mwangaza wa jua. Kuna sababu nyingine pia. Muundo wa paa hiyo ulionwa kuwa sehemu ya pekee zaidi ya michezo hiyo. Kama vile aliyekuwa waziri wa utamaduni wa Ugiriki, Evangelos Venizelos alivyosema, “paa hiyo ndiyo sehemu ya kuvutia ya ujenzi na inawakilisha michezo ya Olimpiki ya Athens.”
-
-
Michezo ya Olimpiki Yarudi NyumbaniAmkeni!—2004 | Agosti 8
-
-
[Picha katika ukurasa wa 16, 17]
Ujenzi wa paa ya Uwanja wa Olimpiki
[Picha katika ukurasa wa 17]
Mfano mdogo wa paa iliyokamilishwa
[Hisani]
© ATHOC
-