-
Maajabu ya Hekima ya KisilikaAmkeni!—2007 | Julai
-
-
Uwezo Unaozidi Silika
Wanadamu, ambao waliumbwa kwa njia ya kustaajabisha na Mungu, hawaongozwi hasa na silika. Badala yake, sisi ni viumbe wenye uwezo wa kujiamulia mambo kwani tuna dhamiri na uwezo wa kuwapenda watu. (Mwanzo 1:27; 1 Yohana 4:8) Kwa sababu ya kuwa na zawadi hizo zote, tunaweza kufanya maamuzi ya haki na yanayotegemea maadili ambayo nyakati nyingine huonyesha upendo mwingi na kujidhabihu.
Bila shaka, mtazamo na tabia ya mtu hutegemea hasa kanuni za maadili na za kiroho ambazo alifundishwa au hakufundishwa alipokuwa mchanga. Kwa sababu hiyo, watu wanaweza kuwa na maoni yanayotofautiana kuhusu lililo sawa na lililo kosa, kuhusu linalofaa na lisilofaa. Tofauti hizo zinaweza kutokeza kutoelewana, kutovumiliana na hata kuchukiana, hasa ikiwa mambo kama utamaduni, uzalendo, na dini yanahusika.
Ulimwengu ungekuwa bora zaidi ikiwa familia yote ya wanadamu ingefuata viwango vilevile ambavyo vinapatana na maadili na kanuni za Biblia, kama tu sote tunavyofuata sheria zilezile za kiasili zinazoongoza ulimwengu wote! Lakini je, kuna mtu yeyote aliye na uwezo na ujuzi wa kuweka viwango vya kufuatwa ulimwenguni pote? Ikiwa yupo, je, atafanya hivyo? Je, tayari amefanya hivyo? Maswali hayo yatajibiwa katika makala inayofuata.
-
-
Mwongozo Bora Kuliko SilikaAmkeni!—2007 | Julai
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 4, 5]
Mwongozo Wako wa Maadili
Wanadamu wana zawadi yenye thamani, yaani, dhamiri. Kwa sababu hiyo, watu wa kila taifa na kabila, kutia na kila enzi, wamekuwa na sheria za maadili zinazofanana. (Waroma 2:14, 15) Hata hivyo, haimaanishi kwamba dhamiri haiwezi kukuongoza vibaya; inaweza kuathiriwa na dini ya uwongo, falsafa za wanadamu, ubaguzi, na tamaa mbaya. (Yeremia 17:9; Wakolosai 2:8) Hivyo, kama vile rubani anavyohitaji kurekebisha vifaa vyake vya kumwongoza, tunahitaji kuchunguza, na inapohitajika, tunahitaji kurekebisha mwongozo wetu wa kiadili na wa kiroho kulingana na viwango vyenye uadilifu vya “Mpaji-sheria wetu,” Yehova Mungu. (Isaya 33:22) Tofauti na viwango vya maadili vya wanadamu vinavyoweza kubadilika kutoka kizazi kimoja hadi kingine, viwango vikamilifu vya Mungu vinadumu milele. Mungu anasema hivi: “Mimi ni Yehova; sikubadilika.”—Malaki 3:6.
-