-
Kufanya Kazi Katika “Shamba” Kabla ya MavunoMnara wa Mlinzi—2000 | Oktoba 15
-
-
Nuru Zaidi Ilihitajiwa
Je, watu kama vile Henry Grew na George Storrs walielewa ile kweli waziwazi kama tunavyoielewa leo? La. Walifahamu pambano lao kama alivyosema Storrs mwaka wa 1847: “Twapaswa kukumbuka kwamba tumetoka tu kwenye enzi za giza za kanisa; na hatutashangaa hata kidogo tukitambua kwamba tunaona mafundisho fulani ya Babiloni kuwa kweli.”
-
-
Kufanya Kazi Katika “Shamba” Kabla ya MavunoMnara wa Mlinzi—2000 | Oktoba 15
-
-
Vivyohivyo, George Storrs hakuelewa kwa usahihi mambo fulani muhimu. Aliweza kutambua mafundisho bandia yaliyofundishwa na makasisi, lakini nyakati fulani alichukua msimamo ulio kinyume kabisa. Kwa mfano, yaonekana baada ya kukasirishwa sana na imani inayokubaliwa na makasisi kuhusu Shetani, Storrs alipinga wazo la kwamba Ibilisi ni mtu halisi. Alikataa Utatu; hata hivyo, hakuwa na uhakika kama roho takatifu ni mtu ama sivyo hadi alipokaribia kufa. Ingawa George Storrs alitarajia kwamba kurudi kwa Kristo hakungeonekana hapo kwanza, hatimaye alifikiri kwamba kungeonekana.
-
-
Kufanya Kazi Katika “Shamba” Kabla ya MavunoMnara wa Mlinzi—2000 | Oktoba 15
-
-
Yapata mwaka wa 1835, Grew aliandika kijitabu cha maana kilichofunua kwamba mafundisho ya kutokufa kwa nafsi na moto wa mateso si ya Kimaandiko. Alihisi kwamba mafundisho hayo yalimkufuru Mungu.
Kijitabu hicho kingekuwa na matokeo makubwa sana. Mwaka wa 1837, George Storrs mwenye umri wa miaka 40 alipata nakala moja kwenye garimoshi. Storrs alikuwa mzaliwa wa Lebanon, New Hampshire, lakini wakati huo alikuwa anaishi Utica, New York.
Alikuwa mhudumu mashuhuri sana katika Kanisa la Methodisti-Episkopali. Aliposoma kijitabu hicho, alivutiwa kuona jinsi hoja nzuri zilivyotolewa kupinga mafundisho ya msingi ya Jumuiya ya Wakristo, ambayo hakuwa amepata kuyatilia shaka. Hakujua mwandishi wa kijitabu hicho, na alikuja kukutana tu na Henry Grew miaka kadhaa baadaye, mwaka wa 1844, wakati ambapo wote wawili walikuwa wanaishi Philadelphia, Pennsylvania. Hata hivyo, Storrs alichunguza jambo hilo mwenyewe kwa miaka mitatu, na kulizungumzia tu na wahudumu wengine.
Hatimaye, kwa kuwa hakuna mtu aliyeweza kukanusha mambo aliyokuwa akijifunza, George Storrs aliamua kwamba hangeweza kuwa mwaminifu kwa Mungu kama angeendelea kushirikiana na Kanisa la Methodisti. Alijiuzulu mwaka wa 1840 na kuhamia Albany, New York.
Katika masika ya mwanzo-mwanzo wa mwaka wa 1842, kwa muda wa majuma sita, Storrs alitoa mfululizo wa hotuba sita wenye kichwa “Uchunguzi—Je, Waovu Ni Wasioweza Kufa?” Watu walipendezwa sana na hotuba hizo hivi kwamba alizisahihisha na kuzichapisha, na kwa miaka 40 iliyofuata, nakala 200,000 ziligawanywa Marekani na Uingereza. Storrs na Grew walifanya mijadala pamoja kupinga fundisho la kutokufa kwa nafsi.
-
-
Kufanya Kazi Katika “Shamba” Kabla ya MavunoMnara wa Mlinzi—2000 | Oktoba 15
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 28]
Mambo Aliyoamini George Storrs
Yesu alitoa uhai wake kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu.
Habari njema hazijahubiriwa bado (mwaka wa 1871).
Kwa sababu hiyo, mwisho haukuwa karibu wakati huo (mwaka wa 1871). Habari njema zingehubiriwa katika kizazi ambacho kingefuata.
Kutakuwa na watu watakaorithi uhai wa milele duniani.
Kutakuwa na ufufuo wa watu wote waliokufa kabla ya kujifunza. Wale wanaokubali dhabihu ya fidia ya Kristo watapokea uhai wa milele duniani. Wale wanaoikataa wataharibiwa.
Kutokufa kwa nafsi na moto wa mateso ni mafundisho bandia yanayomshushia Mungu heshima.
Mlo wa Jioni wa Bwana ni sherehe ya kila mwaka inayofanywa Nisani 14.
[Hisani]
Picha: SIX SERMONS, by George Storrs (1855)
-