-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Johannes Tshange alirudi kwao Ndwedwe, karibu na Durban. Aliijua kweli ya Biblia, naye aliwahubiria wengine. Aliongoza mafunzo ya Biblia kwa ukawaida na kikundi kidogo, akitumia kitabu Studies in the Scriptures katika Kiingereza.
-
-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Bidii yao ilionekana katika ripoti ya mwaka wa 1915, iliyoonyesha kwamba nakala 3,141 za kitabu Studies in the Scriptures zilikuwa zimegawanywa, mara mbili hivi ya nakala zilizogawanywa mwaka uliotangulia.
Mmoja wa wale waliopata kweli wakati huo ni Japie Theron, wakili stadi. Alisoma katika gazeti la Durban makala iliyokuwa ikizungumzia vichapo vilivyochapishwa na Wanafunzi wa Biblia makumi ya miaka mapema. Makala hiyo ilionyesha kwamba matukio ambayo yamekuwa yakitukia tangu 1914 yalikuwa yametabiriwa katika ule mfululizo wa vitabu Studies in the Scriptures, vilivyokuwa vikifafanua unabii wa Biblia. Japie aliandika hivi: “Niliazimia kuvipata vitabu hivyo, na baada ya kuvitafuta katika maduka yote ya vitabu na kugonga mwamba, mwishowe nilivipata baada ya kuandikia ofisi iliyokuwa Durban. Navyo vilikuwa na ujumbe wenye kusisimua kama nini! Ni shangwe iliyoje kuelewa ‘mambo yaliyofichwa’ ambayo yako katika Biblia!”
-
-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 74]
“Studies in the Scriptures”
-