Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kushukuru kwa Ajili ya Maisha Marefu Katika Utumishi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Oktoba 1
    • BABA hakuwa ameajiriwa kazi mwaka wa 1905, hivyo akaenda Marekani. Alirudi miaka mitatu baadaye akiwa na sanduku lililojaa zawadi zenye kusisimua kwa ajili ya watoto na vitambaa vya hariri na vitu vingine kwa ajili ya mama. Lakini mali zake za thamani zaidi zilikuwa mabuku yaliyoandikwa na Charles Taze Russell yenye kichwa Studies in the Scriptures.

      Baba alianza kuwaambia marafiki na jamaa mambo aliyojifunza kutoka katika vitabu hivyo. Kwenye mikutano ya kikanisa cha mahali hapo, alitumia Biblia kuonyesha kwamba hakuna helo yenye kuwaka moto. (Mhubiri 9:5, 10) Katika 1909, mwaka baada ya baba kurudi kutoka Marekani, Ndugu Russell alizuru Norway na kutoa hotuba Bergen na Kristiania, miji ambayo sasa yaitwa Oslo. Baba alienda Bergen kumsikiliza.

  • Kushukuru kwa Ajili ya Maisha Marefu Katika Utumishi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Oktoba 1
    • “Njoo hapa, Ottilie,” akanitia moyo, “na uone yale ambayo Biblia husema.” Ndipo akanisomea Maandiko. Tokeo ni kwamba, uhakika wangu katika yeye na yale aliyofundisha ulikua. Alinitia moyo nisome vichapo Studies in the Scriptures, kwa hiyo wakati wa kiangazi cha mwaka wa 1914, mara nyingi nilisoma nikiwa nimeketi juu ya kilima chenye kuelekea mjini.

      Agosti 1914 umati ulikusanyika nje ya jengo la magazeti ya habari la mahali hapo wakisoma juu ya kuzuka kwa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza. Baba alikuja na kuona yaliyokuwa yakitukia. “Asante Mungu!” akasema kwa mkazo. Alitambua katika kuzuka kwa hiyo vita utimizo wa unabii mbalimbali wa Biblia ambao alikuwa amehubiri juu yake. (Mathayo 24:7) Wakati huo Wanafunzi wa Biblia wengi waliamini kwamba wangechukuliwa mbinguni upesi. Hilo lilipokosa kutukia, baadhi yao walitamauka.

      Msimamo Wangu kwa Ajili ya Kweli ya Biblia

      Mwaka wa 1915, nikiwa mwenye umri wa miaka 17, nilimaliza shule ya kati na kuanza kufanya kazi ya kimwili ofisini. Kisha nikaanza kusoma Mnara wa Mlinzi kwa ukawaida. Lakini mikutano ya kawaida haikufanywa Kopervik hadi mwaka wa 1918. Mwanzoni, tulihudhuria tukiwa watano. Tulisoma vichapo vya Watch Tower Society, kama vile Studies in the Scriptures, na kuzungumzia habari hiyo kwa njia ya maswali na majibu. Ijapokuwa mama aliwasifu Wanafunzi wa Biblia kwa watu wengine, hakupata kamwe kuwa mmoja wetu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki