-
Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho WaoSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
WAKRISTO WA KWELI WAANGUKA LAKINI WAWA HODARI
3, 4. Ni nani “wafanyao maovu juu ya hilo agano,” nao wamekuwa na uhusiano gani na mfalme wa kaskazini?
3 “Na wao wafanyao maovu juu ya hilo agano,” akasema malaika wa Mungu, mfalme wa kaskazini “atawapotosha kwa maneno ya kujipendekeza.” Kisha malaika akasema hivi: “Lakini watu wamjuao Mungu wao watakuwa hodari, na kutenda mambo makuu. Na hao walio wenye hekima katika watu watafundisha wengi; hata hivyo wataanguka kwa upanga, na kwa moto, na kwa kufungwa, na kwa kutekwa nyara, siku nyingi.”—Danieli 11:32, 33.
-
-
Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho WaoSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
5, 6. “Watu wamjuao Mungu wao” walikuwa nani, na walipatwa na hali gani chini ya mfalme wa kaskazini?
5 Vipi juu ya Wakristo wa kweli—“watu wamjuao Mungu wao” na “wenye hekima”? Ingawa walikuwa “katika ujitiisho kwa mamlaka zilizo kubwa” ifaavyo, Wakristo walioishi chini ya utawala wa mfalme wa kaskazini hawakuwa sehemu ya ulimwengu. (Waroma 13:1; Yohana 18:36) Walikuwa waangalifu kumlipa “Kaisari vitu vya Kaisari,” na kumlimpa “Mungu vitu vya Mungu.” (Mathayo 22:21) Kwa sababu hiyo, uaminifu-maadili wao ulijaribiwa.—2 Timotheo 3:12.
6 Kwa sababu hiyo, Wakristo wa kweli ‘walianguka’ na ‘wakawa hodari.’ Walianguka katika maana ya kwamba walinyanyaswa vikali, hata wengine wakauawa. Lakini walikuwa hodari katika maana ya kwamba walio wengi waliendelea kuwa waaminifu. Waliushinda ulimwengu, kama alivyofanya Yesu. (Yohana 16:33) Isitoshe, hawakuacha kuhubiri, hata ikiwa walifungwa gerezani au kwenye kambi za mateso. Kwa kufanya hivyo, ‘waliwafundisha wengi.’ Licha ya mnyanyaso katika nchi nyingi zilizotawalwa na mfalme wa kaskazini, idadi ya Mashahidi wa Yehova iliongezeka. Kwa sababu ya uaminifu wa “wenye hekima,” “umati mkubwa” unaoongezeka daima umetokea katika nchi hizo.—Ufunuo 7:9-14.
WATU WA YEHOVA WATAKASWA
7. Ni “msaada kidogo” gani ambao Wakristo watiwa-mafuta waliokuwa wakiishi chini ya mfalme wa kaskazini walipokea?
7 Watu wa Mungu “watakapoanguka, watasaidiwa kwa msaada kidogo,” akasema malaika. (Danieli 11:34a) Ushindi wa mfalme wa kusini katika vita ya ulimwengu ya pili ulitokeza utulivu kidogo kwa Wakristo waliokuwa chini ya mfalme wa kaskazini. (Linganisha Ufunuo 12:15, 16.) Hali kadhalika, walionyanyaswa na mfalme aliyetawala baadaye, walipata utulivu pindi kwa pindi. Ile Vita Baridi ilipokuwa ikipungua, viongozi wengi walipata kutambua kwamba Wakristo waaminifu hawakuwa tisho lolote na hivyo wakawapa kibali cha kisheria. Pia, msaada ulitokana na idadi kubwa yenye kuongezeka ya umati mkubwa, walioitikia kuhubiri kwa uaminifu kulikofanywa na watiwa-mafuta na kuwasaidia.—Mathayo 25:34-40.
8. Watu fulani waliambatanaje na watu wa Mungu “kwa maneno ya kujipendekeza”?
8 Baadhi ya wale waliodai kwamba wanapenda kumtumikia Mungu wakati wa ile Vita Baridi hawakuwa na makusudi mazuri. Malaika alikuwa ameonya hivi: “Lakini wengi wataambatana nao kwa maneno ya kujipendekeza.” (Danieli 11:34b) Wengi walipendezwa na kweli lakini hawakutaka kujiweka wakfu kwa Mungu. Lakini wengine ambao walionekana kana kwamba waliikubali kweli, kwa kweli walikuwa wapelelezi wa wenye mamlaka. Ripoti moja kutoka nchi moja yataarifu hivi: “Baadhi ya watu hao wasio wanyoofu walikuwa Wakomunisti sugu na walikuwa wamepenya ndani ya tengenezo la Bwana, wakajionyesha kuwa na bidii nyingi, na hata walikuwa wamewekwa katika vyeo vya juu vya utumishi.”
9. Kwa nini Yehova aliruhusu baadhi ya Wakristo waaminifu ‘waanguke’ kwa sababu ya watu waliopenya ndani ya tengenezo lake?
9 Malaika huyo aliendelea kusema hivi: “Na baadhi yao wenye hekima wataanguka, ili kuwatakasa, na kuwasafisha, na kuwafanya weupe, hata wakati wa mwisho; kwa maana ni kwa wakati ulioamriwa, ambao haujaja.” (Danieli 11:35) Watu hao waliokuwa wamepenya ndani walisababisha waaminifu waanguke mikononi mwa wenye mamlaka. Yehova aliruhusu mambo hayo yatukie ili watu wake watakaswe na kusafishwa. Kama vile Yesu “ali[vyo]jifunza utii kutokana na mambo aliyoteseka,” ndivyo waaminifu hao wamejifunza uvumilivu kwa sababu imani yao imejaribiwa. (Waebrania 5:8; Yakobo 1:2, 3; linganisha Malaki 3:3.) Kwa hiyo, ‘wanatakaswa, kusafishwa, na kufanywa weupe.’
10. Ni nini kinachomaanishwa na maneno “hata wakati wa mwisho”?
10 Watu wa Yehova wangeanguka na kutakaswa “hata wakati wa mwisho.” Bila shaka, wanatarajia kunyanyaswa hadi mwisho wa mfumo huu mwovu wa mambo. Hata hivyo, uvamizi wa mfalme wa kaskazini unaosababisha watu wa mungu kusafishwa na kufanywa weupe ni “kwa wakati ulioamriwa.” Kwa hiyo, kwenye Danieli 11:35, “wakati wa mwisho” lazima uwe mwisho wa kipindi cha wakati kinachohitajiwa ili watu wa Mungu watakaswe huku wakivumilia mashambulio ya mfalme wa kaskazini. Yaonekana kule kuanguka kuliisha kwenye wakati ulioamriwa na Yehova mwenyewe.
-