-
Faida za Kujitiisha Katika Mpango wa KitheokrasiTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
kwa kufanya hivyo. (Yoh. 15:20) Hata hivyo, Yesu alijitiisha kwa Mungu. Yesu “alijinyenyekeza” mpaka “kifo juu ya mti wa mateso.” Kujitiisha kwake kikamili kwa Yehova kulikuwa na faida nyingi. Kuliwaletea wanadamu wokovu wa milele, kulifanya apandishwe cheo, na kulimtukuza Baba yake.—Flp. 2:5-11; Ebr. 5:9.
TUNAPASWA KUJITIISHA KWA NANI?
6 Tunapojitiisha kwa Mungu kwa kufanya mapenzi yake, tunaepuka mahangaiko na mambo mengi yenye kuvunja moyo yanayowapata wale wanaokataa kujitiisha chini ya enzi kuu ya Yehova. Adui yetu, Ibilisi, hujaribu kila wakati kutumeza. Tutakombolewa kutoka kwa mwovu huyo ikiwa tutachukua msimamo dhidi yake na kujinyenyekeza mbele za Yehova kwa kujitiisha kwake kwa kupenda.—Mt. 6:10, 13; 1 Pet. 5:6-9.
7 Katika kutaniko la Kikristo, tunatambua ukichwa wa Kristo na mamlaka ambayo amempa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” Jambo hilo huathiri jinsi tunavyowaona na kuwatendea wengine kutanikoni. Kujitiisha kwa mpango wa Mungu kutanikoni kutatuchochea kutii Neno la Mungu katika sehemu zote za ibada yetu. Utii huo unatia ndani huduma yetu, kuhudhuria na kushiriki mikutano, uhusiano wetu na wazee, na kuunga mkono mipango ya kitengenezo.—Mt. 24:45-47; 28:19, 20; Ebr. 10:24, 25; 13:7, 17.
8 Kujitiisha kwa Mungu huchangia amani, usalama, na utaratibu mzuri wa kutaniko la Kikristo. Watu wanaojitiisha kwa Mungu huonyesha sifa bora za Yehova. (1 Kor. 14:33, 40) Mambo ambayo tumejionea katika tengenezo la Yehova yametuchochea tuhisi kama Mfalme Daudi. Baada ya kuona tofauti kati ya watumishi wa Yehova na waovu, Daudi aliimba hivi kwa shangwe: “Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!”—Zab. 144:15.
9 Katika mpango wa ndoa na familia, “kichwa cha mwanamke ni mwanamume.” Wakati huohuo, wanaume nao wanapaswa kujitiisha kwa Kristo, nacho Kichwa cha Kristo ni Mungu. (1 Kor. 11:3) Wake wanapaswa kujitiisha kwa waume zao, na watoto kwa wazazi wao. (Efe. 5:22-24; 6:1) Kila mmoja katika familia anapotii kanuni ya ukichwa, kunakuwa na amani.
10 Mume anapaswa kutumia ukichwa kwa upendo, na hivyo kumwiga Kristo. (Efe. 5:25-29) Akitumia vizuri na kutopuuza ukichwa wake, mke na watoto wake hufurahia kujitiisha. Jukumu la mke ni kuwa msaidizi au kikamilisho. (Mwa. 2:18) Anapomheshimu na kumuunga mkono mume wake bila kulalamika, anapata kibali cha mume wake na kumletea Mungu sifa. (1 Pet. 3:1-4) Waume na wake wanapotii shauri la Biblia kuhusu ukichwa, wanawawekea watoto wao mfano mzuri wa kujitiisha kwa Mungu.
Ujitiisho wa kitheokrasi hugusa kila sehemu ya maisha
11 Kujitiisha kwa Mungu huathiri pia mtazamo wetu kuelekea “mamlaka zilizo kubwa,” ambazo “zimewekwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri.” (Rom. 13:1-7) Wakiwa raia wanaotii sheria, Wakristo hulipa kodi, wakimlipa “Kaisari vitu vya Kaisari, na Mungu vitu vya Mungu.” (Mt. 22:21) Pia, mipango ya kuhubiri eneo kikamili hupatana na sheria za kulinda taarifa zinazotumiwa. Tukijitiisha na kuheshimu mamlaka halali katika mambo yote ambayo hayapingani na sheria ya Yehova ya uadilifu, tutatumia vizuri nguvu zetu zote katika kazi ya kuhubiri.—Marko 13:10; Mdo. 5:29.
12 Ujitiisho wa kitheokrasi hugusa kila sehemu ya maisha. Kwa macho ya imani, tunatazamia kuiona siku ambayo wanadamu wote watajitiisha kwa Yehova Mungu. (1 Kor. 15:27, 28) Wale wanaokubali kwa shangwe enzi kuu ya Yehova watabarikiwa sana wanapoendelea kujitiisha kwake kwa umilele wote!
-
-
Undugu Wenye UmojaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
SURA YA 16
Undugu Wenye Umoja
YEHOVA MUNGU alishughulika na Waisraeli kwa miaka 1,500 hivi wakiwa taifa lake. Baadaye, Yehova ‘alielekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake.’ (Mdo. 15:14) Watu kwa ajili ya jina la Yehova wangekuwa mashahidi wake, nao wangefikiri na kutenda kwa umoja popote walipo duniani. Kazi ambayo Yesu aliwapa wafuasi wake ingetokeza kukusanywa kwa watu kwa ajili ya jina la Mungu. Aliwaagiza hivi: “Basi, nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mkiwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na kuwafundisha kushika mambo yote niliyowaamuru.”—Mt. 28:19, 20.
Wewe ni sehemu ya undugu wa ulimwenguni pote wa Wakristo wenye umoja ambao hawatenganishwi na tofauti za kitaifa, kikabila, au kiuchumi
2 Umekuwa mwanafunzi wa Yesu Kristo kwa kujiweka wakfu kwa Yehova na kubatizwa. Wewe ni sehemu ya undugu wa ulimwenguni pote wa Wakristo wenye umoja ambao hawatenganishwi na tofauti za kitaifa, kikabila, au kiuchumi. (Zab. 133:1) Kwa sababu hiyo, unawapenda na kuwaheshimu ndugu zako Wakristo kutanikoni. Huenda zamani usingeweza kushirikiana na baadhi yao kwa sababu ya tofauti za kijamii, kitaifa, au kielimu. Mmeunganishwa kwa upendo wa kindugu ulio imara na wenye nguvu kuliko uhusiano mwingine wowote wa kijamii, wa kidini, au wa familia.—Marko 10:29, 30; Kol. 3:14; 1 Pet. 1:22.
KUBADILI MTAZAMO
3 Ikiwa wengine wanaona ni vigumu kushinda ubaguzi wa rangi, wa kisiasa, wa kitabaka, au ubaguzi wa aina nyingine yoyote, wanaweza kuwafikiria Wakristo Wayahudi wa karne ya kwanza, ambao walihitaji kufanya juu chini ili waache kuwabagua watu wengine ambao hawakuwa wa dini ya Kiyahudi. Petro alipoagizwa aende nyumbani kwa Kornelio, ofisa wa jeshi wa kikosi cha Roma, Yehova alimtayarisha Petro kwa ajili ya mgawo huo kwa njia ya fadhili.—Matendo sura ya 10.
4 Katika maono, Petro aliambiwa achinje na kula wanyama fulani waliokuwa najisi kulingana na desturi za Wayahudi. Petro alipokataa, sauti kutoka mbinguni ilimwambia: “Acha kuviita najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.” (Mdo. 10:15) Mungu alihitaji kuingilia kati ili Petro abadili mtazamo wake kuhusu mgawo ambao angepewa wa kwenda kumtembelea mtu wa mataifa. Alipotii mwelekezo wa Yehova, Petro aliwatangazia hivi wale waliokusanyika: “Mnajua jinsi ilivyo kinyume cha sheria kwa Myahudi kushirikiana au kumkaribia mtu wa jamii nyingine, lakini Mungu amenionyesha kwamba sipaswi kumwita mtu yeyote najisi au asiye safi. Basi nilipoitwa nilikuja bila kupinga.” (Mdo. 10:28, 29) Baadaye, Petro alijionea uthibitisho wa kwamba Yehova alikuwa amemkubali Kornelio na watu wa nyumbani mwake.
5 Sauli wa Tarso, Farisayo mwenye elimu ya juu, alihitaji kujinyenyekeza ili kushirikiana na watu wa jamii ambayo hapo zamani hangekubali kushirikiana nao. Hata alihitaji kukubali mwongozo kutoka kwao.
-