Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Unavyoweza Kupata Mafanikio ya Kweli Maishani
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Desemba 15
    • 6. Mfano wa Sulemani unatusaidiaje kupima mafanikio ya kweli?

      6 Kwa miaka mingi, Sulemani alitembea kwa kumwogopa Mungu. Tunasoma kwamba ‘aliendelea kumpenda Yehova kwa kutembea katika sheria za Daudi baba yake.’ (1 Fal. 3:3) Je, huoni kwamba alifanikiwa kikweli? Akiongozwa na Mungu, Sulemani alijenga hekalu lenye utukufu kwa ajili ya ibada ya kweli na kuandika vitabu vitatu vya Biblia. Ingawa huenda tusifanye mambo hayo aliyofanya Sulemani, mfano alioweka alipokuwa mwaminifu kwa Mungu unaweza kutusaidia kuelewa kufanikiwa kikweli kunamaanisha nini, na tunachohitaji kufanya ili tufanikiwe. Kuhusiana na hilo, kumbuka kwamba roho ya Mungu ilimwongoza Sulemani kuandika kwamba mambo ambayo watu wengi leo huona kuwa kipimo cha mafanikio, yaani, utajiri, hekima, umashuhuri, na mamlaka, yote ni ubatili. Kwa kweli, mambo hayo hayana faida yoyote, ni “kufuatilia upepo.” Je, hujaona kwamba watu wengi wanaopenda utajiri wanatamani kupata mali zaidi? Na mara nyingi wana wasiwasi kuhusu vitu walivyo navyo. Isitoshe, siku moja mali zao zitachukuliwa na watu wengine.—Soma Mhubiri 2:8-11, 17; 5:10-12.

      7, 8. Sulemani alikosa uaminifu jinsi gani, na matokeo yalikuwa nini?

      7 Pia, unajua kwamba hatimaye Sulemani hakuendelea kuwa mwaminifu na mtiifu. Neno la Mungu linasema: “Ikawa kwamba wakati Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakawa wameugeuza moyo wake ukaifuata miungu mingine; na moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Yehova Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake. . . . Sulemani akaanza kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.”—1 Fal. 11:4-6.

      8 Akiwa na sababu ya kuudhika, Yehova alimwambia hivi Sulemani: “Kwa sababu . . . hukushika agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako, nami nitampa mtumishi wako.” (1 Fal. 11:11) Ulikuwa msiba mkubwa kama nini! Ingawa Sulemani alikuwa amefanikiwa katika njia nyingi, baadaye alimhuzunisha Yehova. Sulemani alishindwa kufanya jambo muhimu zaidi maishani, yaani, kubaki mwaminifu kwa Mungu. Kila mmoja wetu anaweza kujiuliza hivi: ‘Je, mimi nimeazimia kuhakikisha kwamba somo ambalo nimejifunza kutokana na maisha ya Sulemani litanisaidia kufanikiwa?’

  • Jinsi Unavyoweza Kupata Mafanikio ya Kweli Maishani
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Desemba 15
    • Haidhuru Paulo alikabili majaribu gani, aliazimia kuwa mwaminifu kwa Mungu na kudumu katika ibada ya kweli licha ya hali ngumu. Huo ndio mradi ambao watu wa ulimwengu hawaufikirii wanapozungumza kuhusu mafanikio.

      12. Kwa nini uliamua kumtumaini Mungu?

      12 Je, una azimio kama la Paulo? Ingawa sikuzote si rahisi kuishi maisha ya uaminifu, tunajua kwamba kuishi kwa uaminifu huleta baraka na kibali cha Yehova, na hilo ndilo humfanya mtu afanikiwe kikweli. (Met. 10:22) Tunafaidika sasa, na bila shaka tunaweza kutarajia baraka wakati ujao. (Soma Marko 10:29, 30.) Kwa hiyo, tuna kila sababu ya kuweka tumaini letu, “si katika utajiri usio hakika, bali katika Mungu, ambaye hutupa sisi vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie.” ‘Tunajiwekea wenyewe kwa usalama hazina ya msingi mzuri kwa ajili ya wakati ujao, ili tuushike imara uzima ulio wa kweli.’ (1 Tim. 6:17-19) Naam, tunaweza kuwa na uhakika kabisa kwamba miaka mia moja kutoka sasa, hata miaka elfu au zaidi inayokuja, tutakumbuka azimio letu na kusema hivi: “Kwa hakika nilichagua njia ya maisha yenye mafanikio ya kweli!”

  • Jinsi Unavyoweza Kupata Mafanikio ya Kweli Maishani
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Desemba 15
    • PATA MAFANIKIO MACHONI PA MUNGU

      17, 18. (a) Mafanikio ya kweli yanategemea nini? (b) Mafanikio hayategemei nini?

      17 Jambo kuu ni hili: Mafanikio ya kweli hayategemei kuwa na ufanisi au cheo machoni pa watu. Mbali na hilo, mafanikio ya kweli hayategemei kuwa na pendeleo fulani katika kutaniko la Kikristo. Ingawa hivyo, baraka kama hiyo inaweza kuhusianishwa na msingi halisi wa mafanikio, yaani, utii na uaminifu wetu kwa Mungu, ambaye anatuhakikishia hivi: “Kinachoangaliwa katika wasimamizi-nyumba ni mtu kupatwa akiwa mwaminifu.” (1 Kor. 4:2) Ni lazima pia tuvumilie ili tuendelee kuwa waaminifu. Yesu alisema hivi: “Yule atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.” (Mt. 10:22) Je, hukubali kwamba kuokolewa ni uthibitisho ulio wazi kabisa wa mafanikio?

      18 Ukitafakari mambo yaliyotajwa hapo juu, unaweza kuona kwamba uaminifu kwa Mungu hauhusiani na umaarufu, elimu, pesa, au cheo katika jamii; wala uaminifu hautegemei kuwa na akili nyingi, uwezo, au vipawa. Katika hali yoyote ile tunayokabili, tunaweza kuthibitika kuwa waaminifu kwa Mungu. Katika karne ya kwanza, baadhi ya watu wa Mungu walikuwa matajiri na wengine walikuwa maskini. Shauri hili la Paulo liliwafaa sana Wakristo matajiri: “Wafanye mema, wawe matajiri katika matendo mazuri, wawe wakarimu, tayari kushiriki.” Wakristo wote, matajiri na maskini, wangeweza ‘kuushika imara uzima ulio wa kweli.’ (1 Tim. 6:17-19) Ndivyo ilivyo leo pia. Sisi sote tuna fursa na daraka lilelile: Ni lazima tubaki waaminifu na kuwa “matajiri katika matendo mazuri.” Tukifanya hivyo, tutafanikiwa machoni pa Muumba wetu na tutakuwa na shangwe kwa sababu tunajua kwamba tunampendeza yeye.—Met. 27:11.

      19. Kuhusu mafanikio, umeazimia nini?

      19 Huenda usiweze kubadili kabisa hali zako, lakini unaweza kuamua jinsi utakavyozishughulikia. Jitahidi kabisa kuwa mwaminifu katika hali zozote unazokabili sasa. Utafaidika sana ukifanya hivyo. Uwe na hakika kwamba Yehova atakubariki sana, sasa na kwa umilele wote. Usisahau kamwe maneno haya ambayo Yesu aliwaambia Wakristo watiwa-mafuta: “Uwe mwaminifu hata kufikia kifo, nami nitakupa taji la uzima.” (Ufu. 2:10) Hayo ndiyo mafanikio ya kweli!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki