-
Ikiwa Muumba Anajali, Mbona Wanadamu Wanateseka Sana?Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
Muda Wazidi Kupita—Kwa Sababu Nzuri
Ili kuelewa ni kwa nini wanadamu wanateseka, ni lazima tutambue kwamba visababishi vya kuteseka ni aksidenti, mielekeo ya dhambi ya wanadamu, hali ya mwanadamu ya kuitumia vibaya dunia, na Shetani Ibilisi. Lakini, haitoshi kujua tu ni kwa nini wanadamu wanateseka. Mtu anapoteseka, ni rahisi kuhisi kama nabii wa kale Habakuki aliposema hivi: “Ee BWANA, nilie hata lini, wewe usitake kusikia? Nakulilia kwa sababu ya udhalimu, ila hutaki kuokoa. Mbona wanionyesha uovu, na kunitazamisha ukaidi? Maana uharibifu na udhalimu u mbele yangu; kuna ugomvi, na mashindano yatokea.” (Habakuki 1:2, 3) Ndiyo, kwa nini Yehova ‘hutazamisha ukaidi’ na haionekani kama anachukua hatua? Akiwa Mweza Yote, yeye ana uwezo na upendo wa haki unaohitajiwa ili kumaliza kuteseka. Basi atafanya hivyo lini?
Kama ilivyotajwa mapema, wenzi wa kwanza wa kibinadamu walipochagua kuwa huru kabisa, Muumba alikuwa na uhakika wa kwamba baadhi ya wazao wao wangetenda kwa njia tofauti. Kwa hekima Yehova aliruhusu wakati upite. Kwa nini? Ili kuthibitisha kwamba utawala bila Muumba hutokeza tu huzuni na, kwa upande mwingine, kuishi kwa kupatana na Muumba ndilo jambo lenye kufaa nalo hutokeza furaha.
Kwa wakati huu, Mungu amedumisha dunia ikiwa mazingira yenye kufurahisha kwa kiasi fulani. Mtume Paulo alisababu hivi: “Katika vizazi vilivyopita yeye aliruhusu mataifa yote yaendelee katika njia zayo, ijapokuwa, kwa kweli, hakujiacha mwenyewe bila ushahidi kwa kuwa alitenda mema, akiwapa nyinyi mvua kutoka mbinguni na majira yenye kuzaa matunda, akijaza mioyo yenu kikamili kwa chakula na uchangamfu.” (Matendo 14:16, 17) Kwa wazi, Muumba hasababishi kuteseka, lakini yeye amekuruhusu ili kutatue masuala muhimu zaidi.
-
-
Ikiwa Muumba Anajali, Mbona Wanadamu Wanateseka Sana?Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 175]
Je, Muda Mrefu Sana Umepita?
Tokea siku za Yobu hadi za Yesu huenda ikaonekana kuwa muda mrefu sana kwa wanadamu kuendelea kuteseka—miaka ipatayo 1,600. Kwa mwanadamu, miaka 100 inaweza kuonekana kuwa muda mrefu sana wa kungoja hadi kuteseka kumalizike. Lakini ni lazima tutambue kwamba masuala makubwa ambayo Shetani alizusha yalimfanya Muumba aonekane vibaya. Kwa maoni ya Mungu kuruhusu kuteseka na uovu ni kwa kipindi kifupi. Yeye ni “Mfalme wa umilele” ambaye kwake ‘miaka elfu machoni pake ni kama siku ya jana ikiisha kupita.’ (1 Timotheo 1:17; Zaburi 90:4) Na kwa wanadamu watakaopewa uhai wa milele, kipindi hiki cha historia ambapo wanadamu waliteseka kitaonekana kama cha muda mfupi sana.
-