-
Ni Nani Msikiaji wa Sala?Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 1
-
-
Hata hivyo, huenda ukajiuliza, ‘Ikiwa Mungu ndiye Muumba mweza-yote, kwa nini ameruhusu wanadamu waendelee kuteseka?’
Yehova amewapa wanadamu uwezo wa kutumia uhuru wa kuchagua, na jambo hilo linatusaidia kujua jinsi Mungu alivyo. Je, hatuthamini uhuru wetu wa kuamua jinsi tutakavyoishi? Lakini kwa kusikitisha, watu wengi wanatumia vibaya uhuru wao na kujisababishia mateso wao wenyewe na wengine pia. Sasa swali la kufikiria kwa uzito ni hili: Mungu ataondoaje kuteseka bila kuwapokonya wanadamu uhuru wao wa kuchagua?
-
-
Kwa Nini Msikiaji wa Sala Anaruhusu Watu Wateseke?Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 1
-
-
Kwa Nini Msikiaji wa Sala Anaruhusu Watu Wateseke?
HATA ingawa watu fulani husali, bado wanashuku ikiwa kuna Mungu. Kwa nini wanatilia shaka? Labda ni kwa sababu wanaona watu wakiteseka sana ulimwenguni. Je, umewahi kujiuliza kwa nini Mungu ameruhusu watu wateseke?
Je, kweli Mungu aliwaumba wanadamu wakiwa katika hali waliyo nayo sasa, yaani, hali ya kutokamilika na kupatwa na mateso? Ingekuwa vigumu kumheshimu mungu ambaye angewaumba wanadamu ili wateseke. Lakini fikiria mfano huu: Ikiwa ungetazama gari jipya huku ukivutiwa nalo, kisha utambue kwamba limeharibika upande mmoja, je, ungefikiria kwamba lilitengenezwa hivyo? Bila shaka, la! Huenda ungefikia mkataa kwamba lilitengenezwa “bila kasoro” na kwamba liliharibiwa na mtu au kitu fulani.
Vivyo hivyo, ikiwa tungetazama na kuvutiwa na mpangilio na ubuni wa ajabu katika mazingira yetu kisha tuone machafuko na ufisadi unaowasumbua wanadamu, tungefikia mkataa gani? Biblia inafundisha kwamba Mungu aliwaumba wanadamu wa kwanza wakiwa wakamilifu lakini baadaye wakajisababishia matatizo. (Kumbukumbu la Torati 32:4, 5) Habari njema ni kwamba Mungu ameahidi kuondoa matatizo hayo kwa kuwarudishia wanadamu watiifu hali yao ya ukamilifu. Hata hivyo, kwa nini amekawia?
Kwa Nini Amekawia Sana?
Jibu linahusiana na swali lililozuka kuhusu ni nani anayepaswa kuwatawala wanadamu. Yehova hakukusudia kamwe wanadamu wajitawale wenyewe. Angekuwa Mtawala wao. Biblia yenyewe inasema: “Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.” (Yeremia 10:23) Jambo la kuhuzunisha ni kwamba wanadamu wa kwanza waliamua kuasi utawala wa Mungu. Kwa kumwasi Mungu, wakawa watenda dhambi. (1 Yohana 3:4) Matokeo ni kuwa walipoteza hali yao ya ukamilifu na wakajisababishia matatizo wao wenyewe na wazao wao pia.
Kwa maelfu ya miaka, Yehova amewaruhusu wanadamu wajitawale, na historia imethibitisha kwamba wanadamu hawana uwezo wa kujitawala wenyewe. Imeonyesha kwamba serikali zote za wanadamu zinasababisha mateso. Hakuna hata moja ambayo imefaulu kuondoa vita, uhalifu, ukosefu wa haki, au magonjwa.
-