-
Kwa Nini Mungu Anawaacha Wanadamu Wateseke?Amkeni!—2006 | Novemba
-
-
Kwa Nini Mungu Hajaingilia Kati?
Kwa kuwashawishi Adamu na Hawa wachague kutomtegemea Muumba wao, Shetani alitokeza familia ambayo haikuwa huru kabisa, bali ilikuwa chini ya mamlaka yake. Familia hiyo, iwe inajua kwamba inaongozwa na “baba” yao Shetani au haijui, ingechagua kufuatia malengo na viwango vyao wenyewe. (Yohana 8:44) Lakini je, maisha ya aina hiyo yangewaletea uhuru wa kweli na furaha ya kudumu? Yehova alijua vizuri kabisa kwamba haingewezekana. Hata hivyo, aliwaruhusu waasi hao wafuate njia waliyochagua, kwa kuwa ni kwa kufanya hivyo tu ndipo masuala yaliyozushwa Edeni yangeweza kusuluhishwa kabisa.
Kwa zaidi ya miaka 6,000, wanadamu wametokeza mfumo wa mambo wa ulimwenguni pote, wakijaribu kila aina ya utawala na sheria. Je, umeridhika na matokeo? Je, wanadamu wana furaha ya kweli, amani, na umoja? Kwa wazi, jibu ni la! Badala yake, vita, njaa, misiba ya asili, magonjwa, na vifo vimekumba wanadamu, na kutokeza “ubatili,” “maumivu,” na “kuugua,” kama tu Biblia inavyosema.—Waroma 8:19-22; Mhubiri 8:9.
Lakini, huenda wengine wakauliza, ‘Kwa nini Mungu hajazuia misiba?’ Kwa wazi, hiyo haingekuwa haki, na ingevuruga suala hilo kwa kufanya ionekane kwamba kumwasi Mungu hakutokezi mambo mabaya. Hivyo, Yehova hajawa akizuia uhalifu na misiba inayotokezwa moja kwa moja au kwa njia isiyo ya moja kwa moja kwa kumwasi yeye.a Yehova hawezi kujihusisha hata kidogo na uwongo wenye kudhuru kwamba mfumo wa Shetani unaweza kufaulu, na kwamba umegundua njia ya kupata furaha! Hata hivyo, Yehova amekuwa akijali mambo yanayotukia. Kwa kweli, amekuwa akitenda, kama tutakavyoona.
-
-
Kwa Nini Mungu Anawaacha Wanadamu Wateseke?Amkeni!—2006 | Novemba
-
-
a Ingawa mara kwa mara Mungu ameingilia mambo ya wanadamu, utendaji wake haujawahi kuunga mkono mfumo huu. Badala ya hivyo, umehusiana na kutimizwa kwa kusudi lake.—Luka 17:26-30; Waroma 9:17-24.
-