-
Afadhali Nijiue?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
-
-
Lakini namna gani ikiwa wewe mwenyewe umekuwa ukifikiria kujiua? Usifiche hisia zako. Zungumza na mtu fulani—mzazi, rafiki, au mtu yeyote anayekujali, atakayekusikiliza, na kuchukulia mambo unayosema kwa uzito. Kwa kuzungumzia matatizo yako waziwazi, hakuna hasara utakayopata, badala yake, utafaidika sana.b
Bila shaka, matatizo yako hayatatoweka kwa kuwa tu umezungumza na mtu fulani. Hata hivyo, huenda msaada mkubwa unaohitaji ni kuzungumza na mtu unayeweza kumtumaini ili akusaidie kuiona hali yako kwa njia inayofaa. Huenda hata kufanya hivyo kukakusaidia kutafuta njia nzuri ya kutatua hali.
-
-
Afadhali Nijiue?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
-
-
Faida ya Sala
Njia ya maana zaidi ya kupashana habari ni kusali. Unaweza kusali kama Daudi: “Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu. Unichunguze, na uzijue fikira zangu zinazofadhaisha, na uone kama ndani yangu mna njia yoyote yenye kuumiza, na uniongoze katika njia ya mpaka wakati usio na kipimo.”—Zaburi 139:23, 24.
Sala si kama gongo tu la kujitegemeza, kama linalotumiwa na walemavu. Ni njia halisi ya kupashana habari na Baba yako wa mbinguni, anayetaka ‘ummiminie moyo wako.’ (Zaburi 62:8) Fikiria kweli za msingi zifuatazo kumhusu Mungu:
● Anafahamu hali zinazokutaabisha.—Zaburi 103:14.
● Anakujua vema kuliko unavyojijua.—1 Yohana 3:20.
● ‘Anakujali wewe.’—1 Petro 5:7.
● Katika ulimwengu wake mpya, Mungu “atafuta kila chozi” kutoka katika macho yako.—Ufunuo 21:4.
Tatizo Linapotokana na Ugonjwa
Kama ilivyotajwa mapema, mara nyingi hisia za kutaka kujiua zinatokana na ugonjwa fulani. Ikiwa unaugua ugonjwa fulani, usiaibike kutafuta msaada. Yesu alisema kwamba wenye kuugua wanahitaji tabibu. (Mathayo 9:12) Inapendeza kwamba magonjwa mengi yana tiba. Na matibabu yanaweza kukufanya uhisi vema zaidi!c
-