-
Kwa Nini Nisijiue?Amkeni!—2008 | Mei
-
-
Umuhimu wa Sala
Njia muhimu zaidi ya mawasiliano unayoweza kuwa nayo ni sala. Unaweza kusali kama Daudi: “Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu. Unichunguze, na uzijue fikira zangu zinazofadhaisha, na uone kama ndani yangu mna njia yoyote yenye kuumiza, na uniongoze katika njia ya mpaka wakati usio na kipimo.”—Zaburi 139:23, 24.
Sala si njia tu ya kukabiliana na matatizo. Ni mawasiliano halisi na Baba yako wa kimbingu, anayetaka ‘ummiminie moyo wako.’ (Zaburi 62:8) Fikiria kweli za msingi zifuatazo kumhusu Mungu:
◼ Anafahamu hali zinazokutaabisha.—Zaburi 103:14.
◼ Anakujua vema kuliko unavyojijua.—1 Yohana 3:20.
◼ ‘Anakujali wewe.’—1 Petro 5:7.
◼ Katika ulimwengu wake mpya, Mungu “atafuta kila chozi” kutoka katika macho yako.—Ufunuo 21:4.
-
-
Kwa Nini Nisijiue?Amkeni!—2008 | Mei
-
-
Lakini vipi ikiwa wewe mwenyewe umefikiria kujiua? Dakt. McCoy anahimiza hivi: “Tafuta msaada, mwambie mtu fulani jinsi unavyohisi—mzazi, mtu wa ukoo, rafiki, mwalimu, mhudumu wa kidini—mtu anayekujali, ambaye atakuchukua kwa uzito, atakusikiliza, na kuwafanya watu wengine muhimu kwako wasikie yale unayohitaji kusema.”
Hutajidhuru bali utanufaika sana kwa kuzungumzia matatizo yako. Fikiria mfano mmoja wa Biblia. Wakati mmoja maishani mwake, mtu mwadilifu Ayubu alisema hivi: “Nafsi yangu inahisi kuchukizwa na uhai wangu.” Lakini akaongeza: “Nitaonyesha hangaiko langu kujihusu mwenyewe. Nitasema kwa uchungu wa nafsi yangu!” (Ayubu 10:1) Ayubu alikata tamaa, naye alihitaji kuzungumza kuhusu maumivu yake. Huenda ukapata kitulizo fulani kwa kuzungumza na rafiki aliyekomaa.
Wakristo wanaotaabika wana msaada mwingine—wazee wa kutaniko. (Yakobo 5:14, 15) Bila shaka, kuzungumza kuhusu matatizo yako hakutafanya matatizo hayo yatokomee. Lakini kuyazungumzia kunaweza kukusaidia kuwa na maoni mazuri kuyahusu, na huenda utegemezo wa mtu unayemtumaini ndicho kitu tu unachohitaji ili kuyasuluhisha.
-