-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Karibu mwezi mmoja baadaye—mnamo Juni 14, Siku ya Bendera ya kila mwaka ya taifa—Mahakama Kuu Zaidi tena ilibadili uamuzi wayo, wakati huu kuhusiana na uamuzi katika kesi ya Gobitis, wakifanya hivyo katika kesi iliyoitwa West Virginia State Board of Education v. Barnette.c Iliamua kwamba “hakuna ofisa, wa juu au wa chini, awezaye kuonyesha yale yanayokubalika na ya kweli katika siasa, utukuzo wa taifa, dini, au mambo mengineyo au kuwalazimisha raia waungame kwa maneno au watende kupatana na imani yao.” Hoja nyingi zilizotolewa katika uamuzi huo zilitumiwa baadaye nchini Kanada na Mahakama ya Rufani ya Ontario katika kesi ya Donald v. Hamilton Board of Education, na Mahakama Kuu Zaidi ya Kanada ilikataa kubatilisha uamuzi huo.
Kupatana na uamuzi wayo katika kesi ya Barnette, na katika siku hiyohiyo, katika kesi ya Taylor v. State of Mississippi,d Mahakama Kuu Zaidi ya Marekani iliamua kwamba Mashahidi wa Yehova hawangeweza kwa kufaa kushtakiwa uhaini kwa kueleza sababu zao za kutosalimu bendera na kwa kufundisha kwamba mataifa yote yako upande wa ushinde kwa sababu yanapinga Ufalme wa Mungu. Maamuzi hayo pia yalitayarisha njia kwa maamuzi yaliyofuata yenye kupendeleka katika mahakama nyinginezo katika kesi zilizohusu wazazi Mashahidi ambao watoto wao walikuwa wamekataa kusalimu bendera shuleni, pamoja na katika masuala yaliyohusu uajiri na utunzi wa watoto. Hali ilikuwa imebadilika kabisa.e
-
-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 687]
Matukio Yaliyotangulia Kubadilishwa kwa Uamuzi
Katika 1940, wakati Mahakama Kuu Zaidi ya Amerika ilipoamua, katika kesi ya “Minersville School District v. Gobitis,” kwamba watoto wa shule wangetakiwa kusalimu bendera, mahakimu wanane kati ya tisa waliunga mkono uamuzi huo. Ni Hakimu Stone pekee aliyepinga. Lakini miaka miwili baadaye, walipokuwa wakiandikisha tofauti zao katika kesi ya “Jones v. Opelika,” mahakimu wengine watatu (Black, Douglas, na Murphy) walitumia pindi hiyo kusema kwamba waliamini kwamba kesi ya “Gobitis” ilikuwa imeamuliwa vibaya kwa sababu ilikuwa imeshusha uhuru wa kidini. Hiyo ilimaanisha kwamba mahakimu wanne kati ya tisa waliunga mkono kubadilishwa kwa uamuzi katika kesi ya “Gobitis.” Mawakili wawili kati ya wale watano waliokuwa wamepuuza uhuru wa kidini walistaafu. Kulikuwa na wengine wawili wapya (Rutledge na Jackson) wakati kesi iliyofuata ya kusalimu bendera ilipopelekwa kwenye Mahakama Kuu Zaidi. Katika 1943, katika kesi ya “West Virginia State Board of Education v. Barnette,” wote wawili waliunga mkono uhuru wa kidini badala ya jambo la kushurutishwa kusalimu bendera. Hivyo, huku mahakimu 6 dhidi ya 3 zikiunga mkono, mahakama ilibadilisha msimamo iliyokuwa imechukua katika kesi tano za mapema (“Gobitis,” “Leoles,” “Hering,” “Gabrielli,” na “Johnson”) zilizokuwa zimekatwa rufani katika Mahakama hiyo.
Kwa kupendeza, katika kupinga uamuzi wa kesi ya “Barnette,” Hakimu Frankfurter alisema hivi: “Kama vile imekuwa katika nyakati zilizopita, Mahakama itabadilisha msimamo wayo mara kwa mara. Lakini ninaamini kwamba Mahakama hii haijapata kamwe kubatilisha maamuzi yayo ili kupunguza uwezo wa serikali ya kidemokrasia, kabla ya kesi hizi za Mashahidi wa Yehova (isipokuwa mabadiliko madogomadogo yaliyopatikana baadaye).”
-
-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 686]
Mahakimu wa Mahakama Kuu Zaidi ya Marekani ambao, 6 dhidi ya 3 walikataa jambo la kushurutishwa kusalimu bendera katika kesi ya “Barnette,” wakiunga mkono uhuru wa ibada. Hiyo ilibatilisha uamuzi wa mapema wa Mahakama iyo hiyo katika kesi ya “Gobitis”
-