-
Jina la Mungu Lajulishwa Katika KiswahiliMnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 1
-
-
Jambo la kupendekeza ni kwamba baadhi ya tafsiri hizo za mapema zilikuwa na jina la Mungu, si katika sehemu chache tu bali katika sehemu zote za Maandiko ya Kiebrania! Watafsiri waliokuwa Zanzibar walitafsiri jina la Mungu kuwa “Yahuwa,” ilihali watafsiri waliokuwa Mombasa walitafsiri kuwa “Jehova.”
Kufikia mwaka wa 1895 Biblia nzima ilikuwa inapatikana katika Kiswahili. Miongo kadhaa baadaye tafsiri nyingine zilichapishwa, ingawa baadhi ya tafsiri hizo hazikusambazwa sana. Mwanzoni mwa karne ya 20, jitihada nyingi zilifanywa ili kufanya Kiswahili cha Afrika Mashariki kilingane katika nchi zote. Jitihada hizo ziliwezesha Biblia tafsiri ya Union Version ichapishwe katika mwaka wa 1952. Hiyo ndiyo tafsiri iliyosambazwa zaidi. Pia, jitihada hizo zilifanya “Yehova” kuwa tafsiri iliyokubaliwa ya jina la Mungu katika Kiswahili.
Inasikitisha kwamba kadiri tafsiri hizo za kale zilivyoacha kuchapishwa, ndivyo jina la Mungu lilivyoacha kutumiwa. Baadhi ya watafsiri wa hivi karibuni wameondoa jina hilo kabisa, na wengine wameliacha katika sehemu kadhaa tu. Kwa mfano, katika tafsiri ya Union Version, jina la Mungu linapatikana mara 15 peke yake, na katika nakala ya mwaka wa 2006 iliyofanyiwa marekebisho, jina hilo linapatikana mara 11 tu.b
Ingawa jina la Mungu limeondolewa karibu kila mahali katika tafsiri hiyo, bado ina jambo fulani lenye kupendeza. Kwenye mojawapo ya kurasa za kwanza-kwanza, kuna maneno yanayosema waziwazi kwamba jina la Mungu ni Yehova. Jambo hilo limewasaidia sana wale wanaotafuta kweli wajifunze kwa kutumia nakala zao wenyewe za Biblia jina la kibinafsi la Baba yetu wa mbinguni.
-