-
“Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
17 Katika 1918 jamii ya Yohana ya Wakristo wapakwa-mafuta—kama kundi hilo mathubuti katika Filadelfia—ilikuwa sharti ikabili upinzani kutoka “sinagogi la Shetani” la ki-siku-hizi. Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, ambao hudai kuwa Wayahudi wa kiroho, waliongoza kwa hila watawala wakandamize Wakristo wa kweli.
-
-
“Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
19. Jamii ya Yohana ilishughulikiaje madaraka ambayo ilipewa na Yesu katika 1919, kukiwa na tokeo gani?
19 Tangu 1919 na kuendelea mabaki ya wapakwa-mafuta, wakifuata kielelezo cha Yesu, walianzisha kampeni yenye bidii ya kutangaza kotekote habari njema za Ufalme. (Mathayo 4:17; Warumi 10:18) Kama tokeo, wengine wa lile sinagogi la Shetani la ki-siku-hizi, Jumuiya ya Wakristo, walijia baki hili la wapakwa-mafuta, wakatubu na ‘wakainama,’ wakikiri mamlaka ya mtumwa huyo. Wao vilevile walikuja kutumikia Yehova katika muungano na wale wazee-wazee wa jamii ya Yohana. Hilo liliendelea mpaka hesabu kamili ya ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu wakakusanywa.
-