Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Joseph McGrath na Cyril Charles walitumwa kwenye eneo la Amis katika Taiwan katika 1949. Walijipata wakiishi katika nyumba zenye paa za nyasi na sakafu za udongo. Lakini kusudi lao la kuwa huko lilikuwa kusaidia watu. Baadhi ya watu wa kabila la Waamis walikuwa wamepokea fasihi za Watch Tower, wakapendezwa na yale waliyosoma, na wakashiriki habari njema na wengine. Sasa wamishonari walikuwa huko kuwasaidia wakue kiroho. Waliambiwa kwamba watu 600 walipendezwa na kweli, lakini jumla ya 1,600 walihudhuria mikutano waliyofanya walipohama kutoka kijiji hadi kijiji. Watu hao wanyenyekevu walikuwa na nia ya kujifunza, lakini walikosa ujuzi sahihi wa mambo mengi. Kwa saburi ndugu walianza kuwafunza, wakikazia somo moja kwa wakati mmoja, mara nyingi wakitumia muda wa saa nane au zaidi katika mazungumzo ya maswali na majibu juu ya mambo fulani kwenye kila kijiji. Mazoezi yaliandaliwa pia kwa wale 140 walioonyesha tamaa ya kushiriki katika kutoa ushahidi nyumba hadi nyumba. Hilo lilikuwa ono la kupendeza jinsi gani kwa wamishonari! Lakini mengi bado yalihitaji kufanywa ikiwa kungekuwa na ukuzi imara wa kiroho.

      Karibu miaka 12 baadaye, Harvey na Kathleen Logan, wamishonari waliozoezwa Gileadi waliokuwa wakitumikia Japani, walipewa mgawo wa kuandaa msaada zaidi kwa ndugu Waamis. Ndugu Logan alitumia wakati mwingi akiwasaidia waelewe mafundisho na kanuni za msingi za Biblia na mambo ya kitengenezo. Dada Logan alifanya kazi pamoja na dada Waamis katika utumishi wa shambani kila siku, baada ya hapo akijitahidi kujifunza kweli za msingi za Biblia pamoja nao. Halafu, katika 1963, Watch Tower Society ilipanga kwamba wajumbe kutoka nchi 28 wakusanyike pamoja na Mashahidi wenyeji huko katika kijiji cha Shou Feng, kuhusiana na mkusanyiko wa ulimwenguni pote. Yote hayo yalianza kuweka msingi imara kwa ajili ya ukuzi zaidi.

  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Picha katika ukurasa wa 536]

      Harvey Logan (mbele katikati) pamoja na Mashahidi Waamis mbele ya Jumba la Ufalme, katika miaka ya 1960

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki