Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa Nini Watu Hawana Subira?
    Amkeni!—2012 | Desemba
    • [Picha katika ukurasa wa 4]

      Wachanganuzi fulani wanasema kwamba katika miaka ya hivi karibuni teknolojia ndiyo imewafanya watu wakose subira. Kulingana na gazeti The Gazette la Montreal, Kanada, watafiti fulani wanasema kwamba “teknolojia kama vile simu za mkononi, kamera, barua-pepe, na iPod zinabadili maisha yetu . . . Matokeo ya papo kwa hapo tunayopata kutoka kwa teknolojia hizo yamefanya tutake kutimiziwa haraka mahitaji yetu katika sehemu nyingine za maisha.”

      Baada ya kufanya uchunguzi, Mwanasaikolojia, Dakt. Jennifer Hartstein, anasema kwamba “tumekuwa jamii ambayo inataka mahitaji yake yatimizwe papo hapo, na tunatazamia mambo yafanywe haraka, kwa njia bora na kwa njia tunayotaka. Mambo yasipofanywa kwa njia hiyo, sisi huudhika na kukasirika, [dalili] ya kukosa subira.” Anaongezea kusema, “Tumepoteza uwezo wa kutulia na kufurahia maisha.”

      Watu fulani wanaamini kwamba barua-pepe zinapoteza umaarufu wake na hivi karibuni zitaacha kutumiwa. Kwa sababu gani? Kwa sababu watu wengi wanaoandika barua-pepe hawana subira ya kungojea jibu kwa saa nyingi, au hata kwa dakika kadhaa. Pia, lazima mtu aanze kwa salamu na kumaliza kwa salamu anapoandika barua na barua-pepe. Lakini watu wengi wanaona jambo hilo kuwa linachosha na linapoteza wakati. Wanapendelea kuandika ujumbe wa haraka ambao hauhitaji mtu afuate adabu zinazohitajika kama anapoandika barua-pepe. Inaonekana kwamba watu wengi hawana wakati wa kupoteza wa kuandika salamu. Watu wengi hawatengi wakati wa kupitia yale waliyoandika ili kuyasahihisha. Kwa sababu hiyo, watu wanapokea barua na barua-pepe ambazo hazikukusudiwa kwa ajili yao au zilizo na makosa mengi ya kisarufi na ya maandishi.

  • Kwa Nini Watu Hawana Subira?
    Amkeni!—2012 | Desemba
    • Wataalamu wamegundua kwamba watu wengi hawana subira ya kusoma habari ndefu zilizochapishwa. Kwa nini? Kwa sababu wamezoea kupitia haraka-haraka kurasa kwenye Intaneti, wakiruka kutoka jambo moja kuu hadi lingine wakitafuta jambo kuu wanalotaka.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki